Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 4:36 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

36 Muvunaji anakwisha kupokea mushahara, naye anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele, kusudi mupandaji na muvunaji wafurahi pamoja.

Gade chapit la Kopi




Yoane 4:36
20 Referans Kwoze  

Wandugu zangu, ninataka mujue kwamba mara nyingi nilikusudia kuwatembelea, lakini mpaka sasa ninapata vizuizo. Ningetamani kupata matunda ya kazi yangu katikati yenu vilevile, kama inavyokuwa katikati ya watu wa mataifa mengine.


Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.


Wale wenye hekima watangaa kama vile anga linavyongaa, na wale waliowaongoza wengine kutenda mema, watangaa kama nyota milele.


Tunda la mwenye haki ni muti wa uzima, na mwenye hekima anavuta watu.


Ujiangalie wewe mwenyewe na kuangalia mafundisho yako, nawe ushikamane nayo. Kwa maana ukifanya hivi, utajiokoa wewe mwenyewe na kuokoa wale wanaokusikiliza.


Ninyi peke yenu tu ndio tumaini, furaha, na taji ya ushindi tutakavyojivunia wakati Bwana Yesu Kristo atakaporudia.


Faida mwovu anayopata ni ya uongo, lakini anayetenda mema, hakika atapata faida.


Na kila mutu aliyeacha nyumba yake, kaka, dada, baba, mama, watoto au mashamba kwa ajili yangu, atapokea mara nyingi zaidi na kupewa uzima wa milele.


Anayemwamini Mwana yuko na uzima wa milele. Anayekataa kumwamini Mwana hatapata uzima; atakaa akipatwa na kasirani ya Mungu.”


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”


“Kweli, kweli ninawaambia: anayesikia neno langu na kumwamini yule aliyenituma, anapata uzima wa milele. Yeye hatahukumiwa, lakini ameponyoka lufu na kupata uzima.


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Kwa maana mushahara wa zambi ni kifo, lakini zawadi Mungu anayotoa ni uzima wa milele kwa kuungana na Yesu Kristo, Bwana wetu.


Ingekuwa nimechagua kazi hii kwa mapenzi yangu mwenyewe, ningeweza kungojea kupokea mushahara. Lakini kwa kuwa ni muzigo niliopewa, inanipasa kuitimiza.


Basi mushahara wangu ni gani? Mushahara wangu ni kutangaza Habari Njema bila kulipwa, maana yake bila kudai haki ninazostahili kwa kuitangaza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite