Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Upepo unavuma pahali unapotaka, nawe unasikia sauti yake, lakini haujui pahali unapotoka wala unapokwenda. Na ni vile inavyokuwa kwa kila mutu anayezaliwa kwa Roho.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 3:8
21 Referans Kwoze  

Hakuna mutu anayeweza kujua mawazo ya mutu mwingine isipokuwa tu roho ya mutu inayokuwa ndani yake. Vilevile, hakuna anayejua mawazo ya Mungu isipokuwa Roho wa Mungu tu.


Mara moja uvumi uliokuwa kama upepo unaovuma kwa nguvu sana ukashuka kutoka mbinguni. Nao ukajaa ndani ya nyumba yote walimokuwa wakiikaa.


Halafu, Yawe akaniambia: Ewe mwanadamu, kwa ajili yangu toa unabii kwa upepo, uuambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ewe upepo kuja toka pande zote ine na kuipulizia miili hii iliyokufa kusudi ipate kuishi.


Munajua kwamba Kristo ni mwenye haki, kwa hiyo munapaswa kujua vilevile kwamba kila mutu anayefuata haki ni mutoto wa Mungu.


Walipokwisha kuomba, nafasi ile walipokuwa wakikusanyika ikatikisika. Nao wote wakajazwa na Roho Mutakatifu na kuanza kutangaza Neno la Mungu kwa uhodari.


Ni yule yule Roho mumoja anayetenda mambo hayo yote, akimupa kila mumoja zawadi mbalimbali kama anavyopenda.


Hawakuzaliwa kuwa watoto wa Mungu kwa namna ya kimutu, wala kwa mapenzi ya kimwili, wala kwa mapenzi ya mutu, lakini wamezaliwa na Mungu.


Alituliza ile zoruba kali, nayo mawimbi yakanyamaza.


Aliamuru, akavumisha zoruba kali, ikarusha juu mawimbi ya bahari.


Analeta mawingu kutoka miisho ya dunia, anapiga umeme na kunyesha mvua, anavumisha upepo kutoka gala zake.


Upepo unavuma tokea kusini, unazunguka mpaka kaskazini. Unazungukazunguka katika mwendo wake, kisha unarudia tena katika muzunguko wake siku zote.


Usishangae kwa sababu nimekuambia kwamba sherti ninyi muzaliwe mara ya pili.


Basi Nikodemo akamwuliza: “Maneno haya yanawezekana namna gani?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite