Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 3:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Baba anamupenda Mwana wake, naye ameweka vitu vyote kwa mukono wake.

Gade chapit la Kopi




Yoane 3:35
25 Referans Kwoze  

Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Na zaidi ya hii Baba hahukumu hata mutu mumoja, lakini amemupa Mwana uwezo wote wa kuhukumu,


Kwa maana Baba anamupenda Mwana, anamwonyesha yote anayofanya yeye mwenyewe. Atamwonyesha mambo makubwa zaidi kuliko haya kusudi mupate kushangaa.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Mungu amemupatia Kristo mamlaka juu ya vitu vyote na kumuweka kuwa kichwa cha kanisa.


Yesu alijua kwamba Baba yake ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye mwenyewe alitoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.


aliyepanda mbinguni, na anayekaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, akitawala wamalaika, nao wenye mamlaka na uwezo wanaokuwa katika mbingu.


Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu aliweka vitu vyote chini ya miguu yake.” Ndiyo Maandiko Matakatifu yanasema kwamba alipewa mamlaka juu ya vitu vyote. Lakini maneno haya yanaonyesha wazi kwamba Mungu hahesabiwi katika hili neno “Vyote”, kwa maana ni yeye aliyemupa mamlaka juu ya vitu vyote.


Uniombe nami nitakupa mataifa kuwa urizi wako, na dunia nzima kuwa mali yako.


Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.


Nimekujulisha kwao, na nitaendelea kukujulisha kusudi upendo ule unaokuwa nao kwangu ukuwe ndani yao, nami mwenyewe nikuwe ndani yao.”


Ninaomba nikuwe ndani yao na wewe ndani yangu, kusudi wapate kuwa mumoja kabisa; na dunia ijue kama wewe ndiwe uliyenituma na kwamba unawapenda kama vile unavyonipenda.


Kama vile Baba anavyonipenda, mimi ninawapenda ninyi vilevile. Mukae katika upendo huu.


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Na sauti ikasikilika toka mbinguni, ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa naye sana.”


Muangalie mutumishi wangu ninayemusaidia; muchaguliwa wangu ambaye moyo wangu umependezwa naye. Nimeiweka roho yangu juu yake, naye ataimarisha sheria yangu katika mataifa.


Nilikuwa pamoja naye kama fundi wa kazi, nilikuwa furaha yake kila siku, nikishangilia mbele yake siku zote,


Wakati wanainchi wa Misri walipoanza kuona njaa, wakamulilia mufalme awape chakula. Naye akawaambia Wamisri wote: “Mwende kwa Yosefu; mufanye neno lolote atakalowaambia.”


Zaidi ya hayo, mufalme akamwambia Yosefu: “Mimi ni mufalme wa Misri! Ninasema hivi: mutu yeyote katika inchi nzima ya Misri asiinue mukono wala muguu wake bila ruhusu yako.”


Akapewa mamlaka, utukufu na ufalme, kusudi watu wa makabila yote, mataifa yote na luga zote wamutumikie. Utawala wake ni wa milele na ufalme wake hautaangamizwa hata kidogo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite