Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 3:31 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

31 “Anayetoka juu ni juu ya yote; anayekuwa wa dunia ni wa dunia, naye anasema maneno ya dunia. Anayetoka mbinguni ni juu ya yote;

Gade chapit la Kopi




Yoane 3:31
22 Referans Kwoze  

Yesu akawajibu: “Ninyi munatoka hapa chini, lakini mimi nimetoka juu. Ninyi ni wa dunia hii, lakini mimi si wa dunia hii.


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Wao ni wazao wa babu zetu, na Kristo alizaliwa kimwili katika kizazi chao. Yeye ndiye mukubwa kupita wote na Mungu anayesifiwa kwa milele! Amina.


Maana mukate Mungu anaoupana ni yule anayeshuka toka mbinguni na kuleta uzima katika dunia.”


Manabii wa uongo ni watu wa dunia, ndiyo maana wanasema mambo ya kidunia nao watu wa dunia wanawasikiliza.


Mimi ni ule mukate wa uzima, ulioshuka toka mbinguni. Kama mutu akikula mukate huu ataishi milele. Na mukate nitakaotoa ni mwili wangu, utakaotolewa kusudi dunia ipate uzima.”


Na juu ya nguo yake na paja la muguu wake kulikuwa kumeandikwa jina hili: “Mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.”


aliyepanda mbinguni, na anayekaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu, akitawala wamalaika, nao wenye mamlaka na uwezo wanaokuwa katika mbingu.


anayekuja nyuma yangu. Mimi sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”


Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.


Katika agano la kwanza wanasema juu ya kanuni za ibada na juu ya nafasi ya kuabudia iliyojengwa na watu.


Huyu ndiye niliyesema juu yake kwamba mutu mumoja anakuja nyuma yangu, lakini ananipita kwa sababu alikuwa mbele sijazaliwa.


Yoane alimushuhudia akisema kwa sauti: “Huyu ndiye niliyesema juu yake: ‘Anayekuja nyuma yangu ananipita, kwa sababu alikuwa mbele sijazaliwa.’ ”


Sherti utukufu wake uzidi na wangu upunguke.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite