Naye mufalme wa Israeli akamujibu Yosafati: “Kungali mumoja, Mikaya mwana wa Imula. Yeye tunaweza kumwomba shauri la Yawe. Lakini ninamuchukia sana kwa sababu yeye, hatabiri jambo zuri juu yangu hata kidogo, lakini baya tu.” Yosafati akamwambia: “Si vizuri kwa mufalme kusema hivyo.”
Mikate hiyo ilipokuwa tayari, Tamari akaiopoa kutoka kikaango. Akamupelekea Amunoni, lakini Amunoni alikataa kula, akaamuru kwamba watu wote watoke inje, na wote wakaondoka.
Kisha akaamuka usiku kati, akamutwaa mwana wangu kutoka kwangu wakati mimi niko katika usingizi, akamulalisha kwenye kufua chake. Halafu akatwaa maiti ya mwana wake, akailalisha kwenye kifua changu.