Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 3:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Hukumu inatokana na hivi: mwangaza umekuja katika ulimwengu, lakini watu wanapenda giza kuliko mwangaza, kwa sababu matendo yao ni mabaya.

Gade chapit la Kopi




Yoane 3:19
33 Referans Kwoze  

Yesu akawaambia watu tena: “Mimi ni mwangaza wa dunia. Yeye anayenifuata hatatembea katika giza hata kidogo, lakini atakuwa na mwangaza wa uzima.”


Kwa hivi wale wote wasioamini maneno ya ukweli, waliofurahia mambo mabaya watahukumiwa.


Lakini wapingaji na wale wanaokataa kufuata ukweli, wakifuata uovu, wataangukiwa na kasirani na hasira ya Mungu.


Wao walipenda kusifiwa na watu kuliko kupata sifa inayotoka kwa Mungu.


Nao wanajua kwamba Sheria ya Mungu inasema kwamba watu wanaotenda maneno haya wanastahili kufa. Lakini hata hivi wanaendelea, si kuyafanya tu, lakini kukubaliana na wale wanaoyatenda.


Basi namna gani mutaweza kuamini, ninyi munaopokea sifa kutoka wamoja kwa wengine, lakini hamutafuti sifa inayotoka kwake anayekuwa Mungu peke yake?


Mbele ya yote, mujue kwamba katika siku za mwisho kutakuja watu watakaoishi kufuatana na tamaa zao wenyewe. Watawachekelea ninyi


Yeye alikuwa chemichemi ya uzima, na uzima huu ulikuwa mwangaza kwa watu.


“Mutumishi anayejua mapenzi ya bwana wake, lakini anakosa kujiweka tayari na kutofanya sawa na mapenzi ya bwana yule, atapigwa fimbo nyingi.


Tena imeandikwa kwamba: “Jiwe lile ni la kukwalisha watu, nalo ni la kuwaangusha.” Wamejikwaa kwa sababu hawakuamini neno la Mungu, na hivi ndivyo walivyopanga kwa ajili yao tangu mwanzo.


Watu wa dunia hawawezi kuwachukia ninyi, lakini wananichukia mimi kwa sababu ninashuhudia kwamba matendo yao ni mabaya.


Kama mutu akitaka kufanya mapenzi ya Mungu, atajua kama mafundisho yangu yanatoka kwa Mungu, au kama ninasema kwa mamlaka yangu mwenyewe.


Wakati Wafarisayo waliposikia maneno haya yote wakamuzarau Yesu, kwa sababu walikuwa wapenda feza.


watu wanaoacha njia zenye kunyooka kwa kufuata njia za giza,


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitawasafisha na kuwapima kwa moto kama vile chuma. Ni namna gani zaidi ya kuwatendea hawa watu wangu waovu?


Mwangaza ule uliangaza katika giza, wala giza halikuuzimisha.


Wakati nikingali katika dunia, mimi ni mwangaza wa dunia.”


Sasa ni wakati wa dunia hii kuhukumiwa; sasa mutawala wa dunia hii atashindwa.


Mimi nimekuja katika dunia kama mwangaza, kusudi mutu yeyote anayeniamini asikae katika giza.


mbuni, kirukanjia, dudumizi, aina zote za kipanga,


Kuhani atamwangalia na kama kivimba cheupe ambacho kimefanya nywele zake zikuwe nyeupe na kivimba kile kimegeuka kuwa kidonda kibichi,


Hiyo itakuwa ndiyo azabu itakayolipata taifa la Misri pamoja na mataifa yote yasiyoshiriki kwa sikukuu ya Vibanda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite