Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 3:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Mungu hakumutuma Mwana wake katika ulimwengu kusudi ahukumu ulimwengu, lakini kusudi ulimwengu uokolewe naye.

Gade chapit la Kopi




Yoane 3:17
36 Referans Kwoze  

Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


Kwa maana Mwana wa Mutu alikuja kutafuta na kuokoa yule aliyepotea.”


Kama vile Baba aliyenituma anavyokuwa muzima, nami ninaishi kwa nguvu zake, vilevile anayenikula ataishi kwa nguvu zangu.


Hakika mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mutu anayemwona Mwana na kumwamini apate uzima wa milele, nami nitamufufua siku ya mwisho.”


Yesu akawajibu: “Hii ndiyo kazi ya Mungu: mumwamini yule aliyemutuma.”


Yesu akawaambia tena: “Amani kwenu! Kama vile Baba alivyonituma, mimi ninawatuma ninyi vilevile.”


Yeye ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu, wala si kwa ajili ya zambi zetu tu, lakini kwa ajili ya zambi za watu wote.


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Na ninajua kwamba unanisikia siku zote, lakini ninasema hivi kwa sababu ya watu hawa wanaokusanyika hapa kusudi wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”


lakini mimi ninamujua sababu nilitoka kwake, naye ndiye aliyenituma.”


Musizanie kwamba mimi nitawashitaki kwa Baba. Atakayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye mulimutumainia.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mungenipenda, kwa maana nimetoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini yeye ndiye aliyenituma.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?


Lakini mimi nina ushuhuda mukubwa zaidi kuliko ule uliotolewa na Yoane. Maana sasa mambo ninayofanya ndiyo Baba aliyoniamuru kutimiza, nayo yananishuhudia na kuonyesha kwamba yeye amenituma.


Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.


Ninyi hamuchungi neno lake ndani yenu, kwa sababu ninyi hamumwamini yule aliyetumwa naye.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


“Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [


Kisha wakaondoka kwenda katika kijiji kingine.


Aliyetumwa na Mungu anasema maneno ya Mungu, kwa sababu Mungu anamujaza Roho wake kwa uwingi.


Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.


Mwanamuke yule akamujibu: “Bwana, hakuna mutu.” Basi Yesu akamwambia: “Mimi vilevile sikuhukumu. Ujiendee, lakini usifanye zambi tena.”]


Kama vile ulivyonituma katika dunia, mimi vilevile nimewatuma katika dunia.


Ninaomba nikuwe ndani yao na wewe ndani yangu, kusudi wapate kuwa mumoja kabisa; na dunia ijue kama wewe ndiwe uliyenituma na kwamba unawapenda kama vile unavyonipenda.


Baba mwenye haki, ijapokuwa dunia haikujui, mimi ninakujua na hawa wanajua kwamba ulinituma.


Kwa maana Mwana wa Mutu alikuja kuokoa yule aliyepotea.]


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite