Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 3:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Na zaidi ya hii hakuna mutu aliyepanda mbinguni, isipokuwa Mwana wa Mutu aliyeshuka toka mbinguni.

Gade chapit la Kopi




Yoane 3:13
24 Referans Kwoze  

Ni nani aliyepanda juu mbinguni na kushuka chini? Ni nani aliyekamata upepo katika mukono? Ni nani aliyefunga maji katika kitambaa? Ni nani aliyeweka mipaka yote ya dunia? Jina lake ni nani? Na ni nani jina la mwana wake? Uniambie kama unajua!


Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.


Maana Daudi mwenyewe hakupanda mbinguni, lakini alisema: ‘Bwana wetu Mungu alimwambia Bwana wangu: Ikaa na mamlaka kwa kuume kwangu,


Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.


Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, yeye ni wa dunia, lakini Adamu wa pili alitoka mbinguni.


Yesu alijua kwamba Baba yake ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye mwenyewe alitoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.


Lakini hivi ndivyo inavyosemwa juu ya kuhesabiwa haki kwa njia ya imani: “Usijiulize: ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’ ” (maana yake ni kumushusha Kristo toka kule.)


Basi itakuwa namna gani kama mukimwona Mwana wa Mutu akipanda tena pahali alipokuwa mbele?


“Anayetoka juu ni juu ya yote; anayekuwa wa dunia ni wa dunia, naye anasema maneno ya dunia. Anayetoka mbinguni ni juu ya yote;


Si kusema kwamba kuna mutu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; yeye ndiye aliyemwona Baba.


Nao wakasema: “Huyu si Yesu mwana wa Yosefu? Si tunawajua baba yake na mama yake? Namna gani anaweza kusema sasa kwamba alishuka toka mbinguni?”


Haziko mbinguni hata museme: ‘Nani atakayepanda juu mbinguni kutuletea kusudi tupate kuzisikia na kuzitii?’


Na sasa, Baba, unipe utukufu karibu nawe, utukufu unaokuwa sawa na ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuumbwa kwa dunia.


Yesu akawaambia: “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mungenipenda, kwa maana nimetoka kwa Mungu na sasa niko hapa. Sikukuja kwa mamlaka yangu mwenyewe, lakini yeye ndiye aliyenituma.


Mimi ni ule mukate wa uzima, ulioshuka toka mbinguni. Kama mutu akikula mukate huu ataishi milele. Na mukate nitakaotoa ni mwili wangu, utakaotolewa kusudi dunia ipate uzima.”


Maana mukate Mungu anaoupana ni yule anayeshuka toka mbinguni na kuleta uzima katika dunia.”


Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Kanisa ni mwili wa Kristo, nalo ni utimilifu wa Kristo anayetimiza vitu vyote.


Yesu akamujibu: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu, nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”


Ikiwa hamwamini wakati ninapowaambia maneno ya dunia, namna gani mutaamini kama nikiwaambia maneno ya mbinguni?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite