10 Yesu akawaambia: “Mulete sehemu ya samaki munaotoka kuvua.”
“Hapa kuna mutoto mumoja anayekuwa na mikate mitano ya shayiri pamoja na samaki mbili. Lakini chakula hiki hakitawafalia kitu watu wengi kama hawa.”
Kisha Yesu akatwaa ile mikate, akamushukuru Mungu na kuigawanya kwa watu walioikaa pale. Akawapa samaki vilevile kwa kadiri walivyotaka.
Walipofika inchi kavu wakaona mukate na samaki zinazokuwa juu ya moto.
Basi Simoni Petro akapanda ndani ya chombo, akakokota wavu mpaka inchi kavu. Nao ulikuwa umejaa samaki wakubwa mia moja makumi tano na tatu. Na ijapokuwa walikuwa wengi vile, wavu haukupasuka.
Basi Yesu akawajongelea, akatwaa mukate, akawagawanyia; na kuwapa samaki vilevile.
Nao walipokuwa hawajasadiki bado kwa sababu ya furaha na mushangao, akawauliza: “Muko na chakula chochote hapa?”