18 Basi Maria wa Magdala akaenda kuwapasha wanafunzi habari kama amemwona Bwana, na kwamba amemwambia maneno hayo.
Na hawa ndio waliowapasha habari ile kwa mitume: Maria wa Magdala, Yoana na Maria mama ya Yakobo. Kulikuwa vilevile wanawake wengine pamoja nao.
Kisha Yesu akawaambia: “Musiogope, muende kuwaambia wandugu zangu waende Galilaya, na kule wataniona.”
Siku ya kwanza ya juma asubui mapema, kulipokuwa kungali giza, Maria wa Magdala akaenda kwenye kaburi. Alipofika kule akaona kama jiwe lililofunika kaburi limeondolewa.
Kati yao kulikuwa Maria wa Magdala, Maria mama ya Yakobo na Yosefu, pamoja na mama ya wana wa Zebedayo.
Mama ya Yesu, dada ya mama yake, Maria muke wa Kleopa na Maria wa muji wa Magdala walikuwa wamesimama karibu na musalaba wake.