Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 20:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Yesu akamwambia: “Maria!” Naye akageuka, akasema kwa kiebrania: “Raboni,” maana yake “Mwalimu.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 20:16
26 Referans Kwoze  

Zamu anamufungulia mulango na kondoo wanasikia sauti yake. Naye anawaita kondoo wake kila mumoja kwa jina lake na kuwapeleka inje.


Yesu akageuka, akawaona wakimufuata, akawauliza: “Munatafuta nini?” Wakajibu: “Rabi (maana yake ‘Mwalimu’), unakaa wapi?”


Siku moja, ilipokuwa saa tisa ya muchana, akaona maono. Aliona waziwazi malaika wa Mungu akiingia kwake na kumwambia: “Kornelio!”


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


Watu wale wakamukuta Yesu kule ngambo ya ziwa na kumwuliza: “Mwalimu, ulifika hapa wakati gani?”


Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.


Lakini malaika wa Yawe akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu! Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa!”


Toma akamujibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!”


Munaniita ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ na munasema kweli, maana ni vile ninavyokuwa.


Marta alipokwisha kusema maneno hayo, akaenda kumwita dada yake Maria na kumwambia kwa siri: “Mwalimu amekuja, na anakuita.”


Kule Yerusalema, karibu na mulango wa muji huu unaoitwa “Mulango wa Kondoo,” kuna kisima chenye viingilio vitano vyenye paa. Kisima kile kinaitwa katika Kiebrania “Betesaida.”


Alimwendea Yesu usiku na kumwambia: “Mwalimu, tunajua kama Mungu amekutuma kufundisha, kwa maana hakuna mutu anayeweza kuonyesha vitambulisho hivi unavyoonyesha isipokuwa anaongozwa na Mungu.”


Natanaeli akamwambia tena: “Mwalimu, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Waisraeli.”


Bwana akamujibu: “Marta! Marta! Kwa nini unahangaika na kusumbuka kwa ajili ya vitu vingi?


Lakini mara moja Yesu akasema nao, akiwaambia: “Mujipe moyo, ni mimi! Musiogope!”


Nililala usingizi, lakini moyo wangu ulikesha. Nikasikia mupenzi wangu akipiga hodi. Unifungulie dada, ee mupenzi wangu, muchumba wangu, njiwa yangu, usiyekuwa na kilema chochote. Kichwa changu kimelowana na umande na nywele zangu na manyunyu ya usiku.


Mara tu nilipoachana nao, nikamwona mupenzi wangu wa moyo. Nikamushika wala sikumwacha aondoke, mpaka nilipomupeleka katika nyumba kwa mama yangu, mpaka ndani ya chumba cha yule aliyenizaa.


Kisha Yawe akakuja na kusimama hapo, akamwita Samweli kama pale mbele: “Samweli! Samweli!” Samweli akasema: “Sema, maana mimi mutumishi wako ninasikiliza.”


Yawe akamwita tena: “Samweli!” Samweli akaamuka, akamwendea Eli na kumwambia: “Nimekuja, maana umeniita.” Lakini Eli akamwambia: “Sikukuita mwana wangu, ulale tena.”


Yawe akamwambia Musa: Kwa sababu umepata kukubaliwa mbele yangu, nami ninakujua kwa jina lako, jambo hilihili ulilolisema nitalifanya.


Yawe alipoona kwamba Musa amegeuka kwa kuangalia kichaka, akamwita pale kutoka kichaka: “Musa! Musa!” Musa akaitika: “Niko hapa. Ninasikiliza!”


Kisha Yosefu akasema: “Ninyi wenyewe mumeona kwa macho yenu na hata ndugu yangu Benjamina ameona kwa macho yake kwamba ni mimi mwenyewe Yosefu ninayezungumuza nanyi.


Nyuma ya mambo yale, Mungu alimupima Abrahamu. Mungu alimwita: “Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa.”


Yesu akamwuliza: “Unataka nikufanyie nini?” Yule kipofu akamujibu: “Mwalimu, ninataka nipate kuona.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite