Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yesu alialikwa vilevile kwenye ndoa ile pamoja na wanafunzi wake.

Gade chapit la Kopi




Yoane 2:2
30 Referans Kwoze  

Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Mwanamuke aliyeolewa anafungwa na Sheria katika maisha yake na mume wake wakati mume wake angali muzima. Lakini kama mume wake akikufa, yeye ni huru kuolewa na yule anayetaka, lakini sherti ndoa ikuwe ya kikristo.


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


Basi, kama mukikula au mukikunywa, au mukifanya neno lolote, mufanye yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.


Naye mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokosa kumutendea mumoja wa hawa wanaohesabiwa kuwa wadogo, hamukunitendea mimi.’


Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Hatabishana wala kupiga kelele, wala hakuna atakayesikia sauti yake katika barabara.


Sikiliza, ninasimama kwenye mulango na ninapiga hodi. Kama mutu akisikia sauti yangu na kunifungulia, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye atakula pamoja nami.


Wakati divai ilipomalizika, mama ya Yesu akamwambia: “Hawana divai tena.”


Nyuma ya maneno yale, akaenda Kapernaumu pamoja na mama yake, wandugu zake na wanafunzi wake. Nao wakakaa kule siku chache.


Wanafunzi wake wakakumbuka maneno haya yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Upendo wangu kwa ajili ya nyumba yako unanichoma.”


Wakati Yesu alipokwisha kufufuka, wanafunzi wake wakakumbuka kwamba alikuwa anasema juu ya jambo lile, wakaamini Maandiko Matakatifu na maneno yale aliyosema.


Kisha mambo hayo, Yesu na wanafunzi wake wakaenda Yudea. Akabaki kule pamoja nao na kubatiza.


(Hakika Yesu mwenyewe hakubatiza mutu lakini ni wanafunzi wake.)


(Wakati ule wanafunzi wake walikuwa wamekwenda katika muji kununua vyakula.)


Basi wanafunzi wakaanza kuulizana: “Kuna mutu aliyemuletea chakula?”


Mwanafunzi wake mwingine mumoja anayeitwa Andrea, ndugu ya Simoni Petro, akamwambia:


Walipokwisha kushiba, Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Mukusanye vipande vinavyobaki, kusudi kusipotee kitu.”


Ilipokuwa magaribi, wanafunzi wake wakashuka kwenda kwenye ziwa.


Wengi kati ya wanafunzi wake waliposikia maneno haya, wakasema: “Masemi haya ni magumu. Ni nani anayeweza kuyakubali?”


Basi kwa sababu ya maneno haya, wengi kati ya wanafunzi wake wakamwacha, nao hawakutembea tena pamoja naye.


Kwa hiyo Yesu akawauliza wale wanafunzi kumi na wawili: “Nanyi munataka kwenda vilevile?”


Yesu akawajibu: “Ni mimi peke niliyewachagua ninyi kumi na wawili, lakini ingawa hivi mumoja wenu ni Shetani!”


(Alisema hivi juu ya Yuda mwana wa Simoni Iskariota, kwa maana yeye ndiye atakayemutoa, ijapokuwa alikuwa mumoja wa wale kumi na wawili.)


wandugu za Yesu wakamwambia: “Ondoka hapa, uende Yudea kusudi wanafunzi wako waone matendo unayofanya.


Naye alipomwona, akamuleta Antiokia. Na kwa muda wa mwaka muzima Barnaba na Saulo walikusanyika katika kanisa la kule na wakawafundisha watu wengi. Ni kule Antiokia ndiko wanafunzi waliitwa kwa mara ya kwanza jina la Wakristo.


Wanafunzi wakakusudia kutuma musaada kwa wandugu waamini waliokaa katika jimbo la Yudea, kila mumoja kwa kadiri alivyoweza kutoa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite