Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Siku mbili zilipopita, kulikuwa ndoa katika muji wa Kana, katika Galilaya. Mama ya Yesu alikuwa pale.

Gade chapit la Kopi




Yoane 2:1
17 Referans Kwoze  

Basi Yesu akarudi tena Galilaya katika muji Kana, pahali alipogeuza maji kuwa divai. Kule kulikuwa mukubwa mumoja wa serikali, aliyekuwa na mwana mugonjwa katika muji Kapernaumu.


Simoni Petro, Toma (anayeitwa Pacha), Natanaeli (wa muji Kana katika Galilaya), nao wana wa Zebedayo pamoja na wanafunzi wengine wawili wa Yesu, wote walikuwa pamoja.


Siku iliyofuata Yesu alitaka kwenda Galilaya. Alipomukuta Filipo akamwambia: “Unifuate.”


Yesu alipokuwa hajamaliza kusema na lile kundi la watu, mama yake na wandugu zake wakafika. Walisimama inje wakitaka kusemezana naye.


Anayemupata muke amepata kizuri; ni zawadi kutoka kwa Yawe.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Ndoa inapaswa kuheshimiwa na watu wote, mume na muke wake wanapaswa kujikinga na uchafu, kwa sababu Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati.


Kesho yake Yoane alikuwa pale tena pamoja na wawili kati ya wanafunzi wake.


Nyumba na mali ni urizi mutu anaopata kwa babu zake, lakini muke mwenye akili anatoka kwa Yawe.


Eburoni, Rehobu, Hamoni, Kana mpaka Sidona muji mukubwa.


Ni vile Yesu alivyofanya kitambulisho chake cha kwanza katika Kana ya Galilaya. Pale alionyesha utukufu wake na wanafunzi wake wakamwamini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite