Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 19:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Basi wakati wale wakubwa wa makuhani na walinzi walipomwona, wakapiga kelele, wakisema: “Umutundike juu ya musalaba! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawaambia: “Mumutwae ninyi wenyewe na kumutundika, kwa maana mimi sioni sababu ya kumuhukumu.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 19:6
15 Referans Kwoze  

Pilato akawaambia: “Ninyi wenyewe mumukamate na mumuhukumu kufuatana na sheria yenu.” Wakamujibu: “Sisi hatuna ruhusa ya kuua mutu.”


Pilato akatoka tena inje na kuwaambia Wayuda: “Angalia, nitawaletea naye hapa inje kusudi mupate kujua kwamba mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu.”


Ni nani kati ya manabii ambaye babu zenu walikosa kumutesa? Waliwaua wale waliotabiri zamani habari za kuja kwa Mwenye Haki. Na sasa mumemutoa na kumwua.


Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.


Lakini wakapiga kelele wakisema: “Umwue! Umwue! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawauliza: “Munataka nimutundike mufalme wenu juu ya musalaba?” Wakubwa wa makuhani wakajibu: “Sisi hatuna mufalme mwingine isipokuwa Mufalme wa Roma.”


Halafu Pilato akawaambia wakubwa wa makuhani na kundi la watu: “Mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu mutu huyu.”


Basi Pilato alipoona kwamba hataweza kufanya kitu, isipokuwa tu kuongeza fujo, akatwaa maji na kunawa mikono yake mbele ya watu wote, akisema: “Lazima ya damu ya mutu huyu isikuwe juu ya kichwa changu! Maneno haya yanawaangukia.”


Pilato akawauliza tena: “Basi munataka nifanye nini na huyu Yesu anayeitwa Kristo?” Nao wote wakajibu: “Atundikwe juu ya musalaba!”


Lakini Petro akamufuata Yesu kwa mbali, hata akaingia ndani ya upango wa Kuhani Mukubwa. Akaingia katika kiwanja, akaikaa pamoja na walinzi kusudi aone mambo yatakayotokea.


Yuda akatwaa kundi la waaskari pamoja na walinzi waliotumwa na wakubwa wa makuhani na Wafarisayo. Akakuja nao kwenye bustani wakibeba taa, mienge na silaha.


Pilato akamwuliza: “Ukweli ni nini?” Pilato alipokwisha kusema neno hili, akatoka tena inje na kuwaambia Wayuda: “Mimi sioni hata sababu moja ya kumuhukumu mutu huyu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite