Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 19:42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

42 Na kwa kuona siku ile ilikuwa ya matayarisho ya siku ya Sabato ya Wayuda na kaburi lilikuwa karibu, wakamuzika Yesu mule.

Gade chapit la Kopi




Yoane 19:42
10 Referans Kwoze  

Siku ile ilikuwa ya matayarisho ya siku ya Sabato iliyofuata. Kwa sababu hii Wayuda hawakutaka maiti za wale waliotundikwa zibaki juu ya misalaba kwa maana siku ile ilikuwa kubwa sana. Kwa hiyo wakamwomba Pilato ruhusa kwamba miguu ya wale waliotundikwa ivunjwe kusudi wakufe mbio na maiti zao ziondoshwe.


Siku ile ilikuwa siku ya matayarisho ya Pasaka, karibu na saa sita. Pilato akawaambia Wayuda: “Mufalme wenu huyu!”


Kulikuwa bustani pale walipomutundika Yesu, na katika bustani ile kulikuwa kaburi jipya, mulimokuwa hamujazikwa mutu.


Walimuzika pamoja na waovu; katika kifo aliwekwa pamoja na watajiri, ingawa hakutesa watu hata kidogo, wala hakusema neno lolote la udanganyifu.


Kwa maana mumezikwa pamoja na Kristo kwa njia ya ubatizo, nanyi mumefufuliwa vilevile pamoja naye, kwa sababu mumeamini uwezo wa Mungu, aliyemufufua.


Alizikwa na kufufuliwa kwa siku ya tatu kisha kufa kwake kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.


Na wakati walipokwisha kutimiza yote yaliyoandikwa juu yake, wakamushusha toka juu ya musalaba na kumuzika.


Pahali pale Yesu alipotundikwa palikuwa karibu na muji, kwa hiyo Wayuda wengi walisoma andiko lile. Nalo lilikuwa limeandikwa katika Kiebrania, Kilatini na Kigriki.


Kwa maana, kama vile Yona alivyobaki ndani ya tumbo la samaki mukubwa kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku, ndivyo vilevile Mwana wa Mutu atakavyobaki ndani ya udongo kwa muda wa siku tatu, muchana na usiku.


Nimekwisha kama maji yaliyomwangika; mifupa yangu yote imeteguka; moyo wangu ni kama inta, unayeyuka ndani yangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite