Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 19:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Lakini wakapiga kelele wakisema: “Umwue! Umwue! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawauliza: “Munataka nimutundike mufalme wenu juu ya musalaba?” Wakubwa wa makuhani wakajibu: “Sisi hatuna mufalme mwingine isipokuwa Mufalme wa Roma.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 19:15
9 Referans Kwoze  

Lakini wote pamoja wakapiga kelele wakisema: “Umwue mutu huyu na utufungulie Baraba!”


Makutano walimusikiliza Paulo mpaka aliposema maneno yale. Kisha wakasema kwa nguvu: “Mumuteketeze mutu huyu! Mumwue, kwa maana hastahili kuishi!”


Maana wote walimufuata nyuma wakilalamika: “Auawe!”


Basi wakati wale wakubwa wa makuhani na walinzi walipomwona, wakapiga kelele, wakisema: “Umutundike juu ya musalaba! Umutundike juu ya musalaba!” Pilato akawaambia: “Mumutwae ninyi wenyewe na kumutundika, kwa maana mimi sioni sababu ya kumuhukumu.”


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Pilato akawaambia: “Ninyi wenyewe mumukamate na mumuhukumu kufuatana na sheria yenu.” Wakamujibu: “Sisi hatuna ruhusa ya kuua mutu.”


Basi utuambie unafikiri nini: Sheria yetu inaturuhusu kulipa kodi kwa Mufalme wa Roma au hapana?”


Ijapokuwa hawakupata sababu ya kumuhukumu kufa, wakamwomba Pilato awape ruhusa ya kumwua.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite