Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 19:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Yesu akamujibu: “Wewe hauna mamlaka yoyote juu yangu, isipokuwa tu yale uliyopewa na Mungu toka juu. Ni kwa hiyo, yule aliyenitoa kwako anabeba zambi kubwa zaidi.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 19:11
37 Referans Kwoze  

Kila mutu anapaswa kutii wakubwa wenye mamlaka. Maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; nao wakubwa wanaotawala wamesimikwa na Mungu.


Yoane akawajibu: “Hakuna mutu anayeweza kuwa na kitu isipokuwa amekipewa na Mungu.


Mutu huyu alitolewa kwenu kufuatana na mupango uliokusudiwa na kujulikana na Mungu tangu zamani. Nanyi mulimwua, kwa kumutia katika mikono ya wenye zambi wamutundike juu ya musalaba.


Muti uliouona ukiwa mukubwa na wenye nguvu, ambao matawi yake marefu yalifika mbinguni, nao ukionekana kutoka kila pahali katika dunia,


Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.


Basi wakatafuta kumufunga, lakini hakuna mutu aliyemukamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijatimia.


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Hayo yote yalimupata mufalme Nebukadneza.


Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Basi, mutu anayejua kutenda mema wala hayatendi, anafanya zambi.


Kwa maana vitu vyote vinatoka kwake, navyo viko kwa uwezo wake na kwa ajili yake. Atukuzwe hata milele! Amina.


Hivi walitimiza mambo uliyokuwa umekusudia tangu zamani kwa uwezo wako na kwa mapenzi yako.


Wakamufunga, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa liwali Pilato.


Musitegemee kutesa, musijisifie mali ya wizi; kama mali zikiongezeka, musizitegemee.


Yuda, yule aliyekuwa amemutoa, alikuwa amekwisha kuwapa kitambulisho hiki: “Yule nitakayemubusu, ndiye yeye. Mumukamate na mumupeleke, mukimulinda vizuri.”


Alifukuzwa mbali na wanadamu, akili yake ikafanywa kama ya nyama, akaishi na punda wa pori, akakuwa anakula majani kama ngombe, na kulowanishwa na umande wa mbinguni mpaka alipotambua kwamba Mungu Mukubwa ndiye anayetawala juu ya falme za wanadamu, naye anamupa ufalme ule mutu yeyote anayemutaka.


Wakaaji wote wa dunia si kitu; anafanya anavyotaka na viumbe vya mbinguni, na wakaaji wa dunia; hakuna anayeweza kumupinga, au kusema: Unafanya nini?


Yuda akatwaa kundi la waaskari pamoja na walinzi waliotumwa na wakubwa wa makuhani na Wafarisayo. Akakuja nao kwenye bustani wakibeba taa, mienge na silaha.


Yesu akawajibu: “Mungekuwa vipofu, hamungekuwa na zambi. Lakini kwa maana munajidai kwamba munaona, mungali katika zambi.”


Siku zote nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu, ninyi hamukunikamata. Lakini hii ni saa yenu; saa ya utawala wa bwana wa giza.”


Nani anayeweza kusema kusudi kitu kifanyike ikiwa Yawe asipoamuru ikuwe hivyo?


Halafu Kuhani Mukubwa akapasua nguo zake na kusema: “Mutu huyu amemutukana Mungu! Hatuhitaji tena ushuhuda wowote juu yake. Angalia, munatoka kusikia jinsi alivyomutukana Mungu.


Uniokoe katika makosa yangu yote; usikubali wapumbafu wanichekelee.


Ukubwa ni wako, ee Yawe, una nguvu, utukufu, ushindi na mamlaka. Vyote vinavyokuwa mbinguni na katika dunia ni vyako. Ee Yawe, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, uko mukubwa juu ya vitu vyote.


Wakamupeleka kwanza kwa Anasi. Anasi alikuwa mukwe wa Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mukubwa mwaka ule.


Basi Pilato akamwambia: “Hautaki kusema nami? Wewe haujui kama mimi nina mamlaka ya kukufungua na mamlaka ya kukutundika juu ya musalaba?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite