Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 18:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Basi Yesu akiwa mwenye kujua maneno yote yatakayomupata, akawaendea na kuwauliza: “Munamutafuta nani?”

Gade chapit la Kopi




Yoane 18:4
27 Referans Kwoze  

Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.


Yesu akawauliza tena: “Munamutafuta nani?” Nao wakasema: “Yesu wa Nazareti.”


Umenionyesha njia za uzima, utanijaza furaha nitakapokuwa karibu nawe.’


Hata jeshi likinizunguka, moyo wangu hautaogopa kitu; hata nikishambuliwa kwa vita, sitakata tumaini.


Kisha, Yesu akiwa anajua kwamba mambo yote yametimia, akasema hivi kusudi Maandiko Matakatifu yatimie: “Ninasikia kiu.”


(Yesu alijua yule atakayemutoa; ndiyo maana alisema: “Ninyi wote si safi.”)


Lakini kuna wengine kati yenu wasioamini.” (Yesu alisema vile kwa sababu alijua tangu mwanzo wale wasioamini na yule atakayemutoa.)


Kisha akawaambia: “Haya ndiyo maneno niliyowaambia wakati nilipokuwa ningali pamoja nanyi, kwamba sherti yatimizwe maneno yote yaliyoandikwa juu yangu katika Sheria ya Musa, katika maandiko ya manabii na katika Zaburi.”


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Usiku huu ninyi wote mutaanguka kwa ajili yangu, kwa maana imeandikwa hivi katika Maandiko Matakatifu: ‘Nitamwua muchungaji, na kondoo wa kundi watasambazwa.’


Nao walipokuwa wakikula, akasema: “Kweli ninawaambia: mumoja kati yenu atanitoa.”


“Munajua kwamba kumebaki siku mbili mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka, na Mwana wa Mutu apate kutolewa kusudi atundikwe juu ya musalaba.”


Tangia wakati ule Yesu akaanza kuwaambia wanafunzi wake waziwazi kwamba ni sherti kwake kwenda Yerusalema, ateswe kule na wasimamizi wa watu, wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria, auawe, na kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.


Waovu wanakimbia ijapokuwa hawafukuzwi na mutu, lakini wenye haki ni hodari kama simba.


Ninalala na kupata usingizi, ninaamuka tena, maana wewe ni tegemeo langu.


Lakini mimi nikajiuliza ndani ya moyo: “Mutu kama mimi ataweza kukimbia? Mutu kama mimi anahitaji kuingia katika hekalu apate kuponyesha maisha yake? Sitaingia hata kidogo katika hekalu.”


Ninakuapia kwa jina la Yawe, Mungu wako, Mwenye Uzima, kwamba mufalme amekuwa akikutafuta katika dunia yote. Na mufalme yeyote akisema kwamba haujaonekana kule, Ahabu alimutaka huyo mufalme aape na watu wake kwamba kweli hauko.


Kristo aliteswa kimwili. Basi ninyi vilevile mujikaze mupate kuwa na nia kama ile yake. Kwa maana mutu anayevumilia mateso ya mwili, anaachana kabisa na zambi.


Wakamujibu: “Yesu wa Nazareti.” Yesu akawaambia: “Ni mimi.” Na Yuda, yule aliyekuwa amemutoa, alikuwa akisimama pale pamoja nao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite