Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 18:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Nao wakamujibu: “Kama asingekuwa mutenda maovu, tusingemuleta kwako.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 18:30
11 Referans Kwoze  

Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Mungu wa babu zetu, ameonyesha kwamba mutumishi wake Yesu ni mwenye utukufu. Ninyi wenyewe mulimutoa na kumukana mbele ya mutawala Pilato, ijapokuwa Pilato alikuwa ameamua kwamba afunguliwe.


Tokea saa ile Pilato alitafuta njia ya kumufungua Yesu. Lakini Wayuda wakapiga kelele, wakisema: “Ukimufungua mutu huyu, wewe si rafiki wa Mufalme wa Roma. Kila mutu anayejifanya kuwa mufalme, anamupinga Mufalme wa Roma!”


Aliwaambia kwamba Mwana wa Mutu anapaswa kutolewa katika mikono ya wenye zambi, na kutundikwa juu ya musalaba, lakini kwa siku ya tatu kisha kufa, atafufuka.”


Nao wakubwa wa makuhani wakamushitaki Yesu juu ya mambo mengi.


Akawaambia: “Tunapanda kwenda Yerusalema na kule Mwana wa Mutu atatolewa kwa wakubwa wa makuhani na kwa walimu wa Sheria. Nao watamuhukumu auawe na kumutoa katika mikono ya watu wa mataifa mengine.


Kwa hiyo Pilato akawakuta inje, na kuwauliza: “Munamushitaki mutu huyu juu ya nini?”


Pilato akawaambia: “Ninyi wenyewe mumukamate na mumuhukumu kufuatana na sheria yenu.” Wakamujibu: “Sisi hatuna ruhusa ya kuua mutu.”


Mimi ninateswa na kufungwa sawa mutenda maovu kwa sababu ninahubiri Habari Njema hii. Lakini Neno la Mungu halifungwi.


Kati yenu kusikuwe hata mutu mumoja anayeteswa kwa sababu yeye ni mwuaji, mwizi, mutenda mabaya au mwenye kujiingiza katika mambo ya watu wengine.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite