Wakati ule Simoni Petro alikuwa angali pale akiota moto. Basi wakamwuliza: “Wewe vilevile si mumoja wa wanafunzi wa mutu huyu?” Petro akakana, akisema: “Hapana! Mimi si mwanafunzi wake.”
Lakini Petro alisimama inje karibu na mulango. Yule mwanafunzi mwingine, aliyejulikana na Kuhani Mukubwa, akatoka inje, akasema na mwanamuke aliyelinda mulango, naye akamwachilia Petro kuingia ndani.