Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.
Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.
Lakini sisi ni watu wa Mungu. Mutu anayemujua Mungu anatusikiliza; yule asiyemujua Mungu hatusikilizi. Basi ni kwa njia hii tunaweza kutambua tofauti kati ya Roho wa ukweli na roho ya udanganyifu.
“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.
Ninaomba nikuwe ndani yao na wewe ndani yangu, kusudi wapate kuwa mumoja kabisa; na dunia ijue kama wewe ndiwe uliyenituma na kwamba unawapenda kama vile unavyonipenda.
Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.
Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.
Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.
Basi wakamwuliza: “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu: “Hamunijui mimi wala hamumujui Baba yangu. Kama mungenijua mimi, mungemujua Baba yangu vilevile.”
Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.
Wao wenyewe wanaeleza namna mulivyotupokea wakati tulipofika kwenu na namna mulivyoacha kuabudu sanamu na kumurudilia Mungu. Mulifanya vile kusudi mumutumikie Mungu mwenye uzima na wa kweli
Musogee karibu nami musikie jambo hili: Tangu mwanzo mimi sikusema kwa siri, tangu mambo hayo yaanze kutendeka, nimekuwa pale. Sasa, Bwana wetu Yawe amenituma, na kunipa nguvu ya Roho wake.
Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?
Na ninajua kwamba unanisikia siku zote, lakini ninasema hivi kwa sababu ya watu hawa wanaokusanyika hapa kusudi wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”
na kuwaambia: “Anayemupokea mutoto mudogo kama huyu kwa jina langu, ananipokea mimi. Naye anayenipokea mimi, anamupokea yule aliyenituma. Kwa maana yule anayekuwa mudogo kati yenu ndiye anayekuwa mukubwa.”
“Anayemupokea mutoto mudogo kama huyu kwa ajili yangu, ananipokea mimi. Na anayenipokea, hanipokei mimi tu, lakini anamupokea vilevile yule aliyenituma.”
Basi kuelekea lile ulizo juu ya kula nyama za kutambikiwa kwa sanamu za miungu, tunajua kwamba sanamu ni kitu bure katika dunia, na ya kuwa kuna Mungu mumoja peke yake tu.
Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo
Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.
Kwa uwezo wake, Mungu ametujalia mambo yote tunayohitaji katika maisha yetu kusudi tupate kushikamana na kumwabudu yule aliyetuita kushiriki utukufu wa wema wake mwenyewe.
Uzima huu ulipotokea, sisi tuliuona. Kwa sababu hii tunaushuhudia na kuwatangazia habari za huo uzima wa milele, uliokuwa pamoja na Baba na ulioonyeshwa kwetu.
Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.