Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 17:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.

Gade chapit la Kopi




Yoane 17:21
37 Referans Kwoze  

Kwa maana, Kristo ni kama mwili mumoja unaokuwa na viungo vingi. Ijapokuwa viungo vya mwili ni vingi, vinakuwa mwili mumoja tu.


Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.


Kitu cha lazima ni kwamba mukuwe na mwenendo unaolingana na mafundisho ya Habari Njema ya Kristo. Kwa hivi hata kama nikikuja kuwaona au hata kama nisipokuja, nipate tu kusikia kwamba munasimama imara katika nia moja, na kwamba wote pamoja munapigana vita kwa ajili ya imani inayotokana na Habari Njema.


Watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, ikiwa munapendana ninyi kwa ninyi.”


Kundi lote la waamini walikuwa na roho moja na nia moja. Hakuna hata mumoja wao aliyehesabia mali yake kuwa yake mwenyewe, lakini walishirikiana katika vitu vyote.


Wakati huo, Yawe atakuwa ndiye mufalme pekee wa dunia yote; naye atakuwa ndiye Yawe pekee, mumoja tu, na jina lake litakuwa ndilo jina pekee.


kwa maana nimewatangazia maneno yale uliyoniagiza, nao wameyakubali. Wamejua hakika kwamba nilitoka kwako na kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.


Lakini kama nikiyatenda, hata ikiwa hamuniamini mimi, basi mwamini matendo yangu, kusudi mupate kujua kabisa kwamba mimi na Baba ni mumoja, yeye ni ndani yangu, nami ndani yake.”


Mimi na Baba yangu tuko mumoja.”


Kwa hiyo hakuna tena umbalimbali kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kati ya watumwa na watu huru, mwanaume na mwanamuke; kwa maana ninyi wote ni mumoja katika kuungana kwenu na Yesu Kristo.


Wandugu zangu, ninawasihi ninyi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mukuwe na masikilizano kusudi matengano yasikuwe katikati yenu. Muishi katika umoja kabisa mukiwa na nia moja na wazo moja.


Hivi vilevile, sisi tunaokuwa wengi tumekuwa mwili mumoja katika kuungana kwetu na Kristo, na sisi wote ni viungo kila mumoja kwa mwingine.


Nitawapa moyo mumoja na nia moja, wapate kuniheshimu mimi siku zote, kwa faida yao wenyewe na kwa faida ya watoto wao watakaofuata.


Maana kuna washuhuda watatu:


Kila siku walikuwa wakikusanyika pamoja katika hekalu, nao walikula chakula pamoja katika nyumba zao kwa furaha na katika unyenyekevu.


Baba mwenye haki, ijapokuwa dunia haikujui, mimi ninakujua na hawa wanajua kwamba ulinituma.


Niko na kondoo wengine wasiokuwa wa kundi hili. Ninapaswa vilevile kuwaleta, nao watasikia sauti yangu, na kutakuwa kundi moja na muchungaji mumoja.


Wakati huo nitabadilisha luga ya watu, nitawawezesha kusema luga safi kusudi waniite mimi Yawe, na kuniabudu kwa moyo mumoja.


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


kusudi watu wote wamuheshimu Mwana kama vile wanavyomuheshimu Baba. Asiyemuheshimu Mwana, hamuheshimu Baba aliyemutuma.


Mungu hakumutuma Mwana wake katika ulimwengu kusudi ahukumu ulimwengu, lakini kusudi ulimwengu uokolewe naye.


Kama vile ulivyonituma katika dunia, mimi vilevile nimewatuma katika dunia.


Na ninajua kwamba unanisikia siku zote, lakini ninasema hivi kwa sababu ya watu hawa wanaokusanyika hapa kusudi wapate kuamini kwamba wewe ndiwe uliyenituma.”


“Siwaombei hawa tu, lakini ninawaombea vilevile wale watakaoamini kwa sababu ya mafundisho yao.


Lakini anayeungana na Bwana anageuka kuwa mumoja naye kiroho.


Lile tuliloona na kulisikia, ndilo tunalotangaza kwenu vilevile, kusudi mupate kushirikiana nasi. Na huu ushirika wetu ni ule tunaokuwa nao pamoja na Baba na Mwana wake Yesu Kristo.


Watu wa ufalme mumoja wakigombana wao kwa wao, ufalme ule utaanguka.


Na ikiwa Mungu ametukuzwa kwa njia yake, basi Mungu vilevile atamutukuza Mwana kwa njia yake mwenyewe, naye atamutukuza bila kukawia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite