Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 17:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Uwatakase wapate kujitoa kwako kabisa kwa njia ya ukweli, maana yake kwa njia ya neno lako la kweli.

Gade chapit la Kopi




Yoane 17:17
23 Referans Kwoze  

Ninyi mumekwisha kuwa safi kwa kuwa mumeshika maneno niliyowaambia.


Kifungo cha neno lako ni ukweli, maamuzi yako yote ya haki yanadumu milele.


Alifanya hivi kusudi atakase kanisa kwa ajili ya Mungu, akilisafisha kwa maji na kwa neno.


Ninajitoa kwako kabisa mimi mwenyewe kwa ajili yao, kusudi wao vilevile wapate kujitoa kwako kabisa.


Halafu mutajua ukweli, na ukweli utawaweka huru.”


Kwa sababu hiyo, mutupilie mbali mambo yote machafu na matendo ya uovu yanayozidi. Mupokee kwa unyenyekevu neno lile lililopandwa ndani yenu na linaloweza kuwaokoa.


Lakini sisi tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu ninyi wandugu wapendwa wa Bwana. Kwa maana Mungu amewachagua ninyi wa kwanza kuwa watu wake kusudi mupate kuokolewa kwa kutakaswa na Roho Mutakatifu na kwa kuamini maneno ya ukweli.


Nimeshika neno lako ndani ya moyo wangu, kusudi nisikukosee.


Hakika mumesikia habari zake, nanyi mukiwa waamini mumefundishwa kufuatana na ukweli unaokuwa ndani ya Kristo.


Namna gani kijana ataweza kujichunga katika njia safi? Ni kwa kufuatilia neno lako.


Kwa kanuni zako ninapata hekima, kwa hiyo ninachukia kila mwenendo mubaya.


Lakini Yawe anasema: “Kwa sababu wamasikini wanaugua, na wakosefu wanalia, sasa ninasimama, nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”


Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.


Sasa, ee Bwana wangu Yawe, wewe ndiwe Mungu, na maneno yako ni kweli. Umeniahidi mimi mutumishi wako jambo hili jema.


Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.


Yeye hakufanya ubaguzi kati yetu na wao; ametakasa mioyo yao kwa sababu walimwamini.


“Basi hii ndiyo maana ya ule mufano wa mupandaji: mbegu ni mufano wa neno la Mungu.


Lakini sasa munatafuta kuniua ijapokuwa nimewaambia ukweli niliousikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya vile.


Maagizo yako ni ya haki siku zote; unijalie akili nipate kuishi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite