Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 17:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Sikuombi kama uwaondoe katika dunia, lakini ninakuomba uwakinge na yule Mwovu Shetani.

Gade chapit la Kopi




Yoane 17:15
18 Referans Kwoze  

Yawe atakukinga na uovu wote; atayalinda salama maisha yako.


Tunajua kwamba kila mutoto wa Mungu hafanyi zambi, kwa maana Mwana wa Mungu anamulinda, wala yule Mwovu hawezi kumugusa.


Lakini Bwana ni mwaminifu, atawaimarisha na kuwakinga na yule Mwovu.


Kristo alijitoa mwenyewe kwa kutuokoa toka katika zambi zetu, kusudi atukomboe katika dunia hii mbaya ya sasa, kwa mapenzi ya Mungu Baba yetu.


Usituache kuanguka katika majaribu, lakini utuokoe na yule Mwovu. [Kwa maana ufalme, uwezo na utukufu ni vyako hata milele. Amina.]’


Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.


Utusamehe zambi zetu, maana sisi vilevile tunawasamehe wote wanaotukosea, usituache kuingia katika majaribu.’ ”


Nilikulilia wewe, ee Yawe; nilikusihi, ee Yawe:


Tangia sasa nimetayarishiwa zawadi ya ushindi, ndiyo ile taji ya haki, ambayo Bwana anayekuwa Mwamuzi wa haki atakayonipa siku ile ya kurudi kwake. Wala hatanipa mimi peke yangu tu, lakini na wale wote wanaopenda kumwona wakati atakaporudi.


Mutu wa haki akikufa, hakuna mutu anayejali; mutu mwema akihamishwa toka dunia, hakuna mutu anayefikiri na kusema: Mutu huyo mwema amehamishwa kusudi asipatwe na hasara,


na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote, awabariki vijana hawa! Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka, yadumishwe katika vijana hawa; nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”


Lakini munaposema, museme tu: ‘Ndiyo,’ au ‘Hapana,’ kwa maana maneno yanayosemwa zaidi ya hayo yanatoka kwa yule mwovu Shetani.


Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.


Lakini mimi nimekuombea, kusudi usipungukiwe na imani. Nawe utakaponirudilia tena, uwatie wandugu zako moyo.”


Tunajua kwamba sisi ni watoto wa Mungu ingawa dunia yote inatawaliwa na yule Mwovu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite