Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 16:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Sasa ninarudi kwake yule aliyenituma na hakuna mumoja wenu anayeniuliza kwamba ninaenda wapi.

Gade chapit la Kopi




Yoane 16:5
15 Referans Kwoze  

Simoni Petro akamwuliza: “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akamujibu: “Hauwezi kunifuata sasa pahali ninapokwenda, lakini utanifuata nyuma.”


Yesu akasema: “Ningali pamoja nanyi kwa wakati kidogo na kisha nitarudi kwa yule aliyenituma.


Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja katika dunia. Sasa ninaacha dunia na kurudi kwa Baba.”


Mimi nimekutukuza wewe katika dunia kwa kuwa nimemaliza kazi ile uliyonipa.


Kuelekea haki ni kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamutaniona tena.


Tukaze macho yetu kuelekea Yesu mwenye kuanzisha na kukamilisha imani yetu. Kwa sababu alijua furaha atakayopata nyuma, alivumilia kufa juu ya musalaba pasipo kuona haya, na sasa anaikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu kwenye kiti cha kifalme cha Mungu.


Yeye ni kitambulisho cha mwangaza wa utukufu wa Mungu, kwa maana yeye ni mufano kamili pahali ya Mungu mwenyewe, na kwa uwezo wa neno lake analinda vitu vyote. Naye alipokwisha kuwatakasa watu toka katika zambi zao, aliikaa na mamlaka katika mbingu kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo wote.


Yesu alijua kwamba Baba yake ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye mwenyewe alitoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.


“Kunabaki wakati kidogo, ninyi hamutaniona; lakini kisha wakati kidogo mutaniona tena.”


Mumesikia jinsi nilivyowaambia kwamba ninajiendea, lakini nitawarudilia tena. Kama mungenipenda, mungefurahia kujua kwamba ninakwenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mukubwa kuliko mimi.


Basi itakuwa namna gani kama mukimwona Mwana wa Mutu akipanda tena pahali alipokuwa mbele?


Lakini sasa ninarudi kwako, nami ninasema maneno haya nikingali katika dunia, kusudi furaha yangu kubwa kabisa ikuwe ndani yao.


Basi wanafunzi wake wamoja wakasemezana hivi: “Yeye anatuambia kwamba kunabakia wakati kidogo nasi hatutamwona, lakini kisha wakati kidogo tutamwona tena. Vilevile anasema kwamba ni kwa sababu anakwenda kwa Baba yake. Maana ya maneno haya yote ni nini?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite