Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 16:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Watawatenga musiingie katika nyumba za kuabudia. Na kutakuwa wakati ambapo wote watakaowaua watazani kwamba wanamutumikia Mungu.

Gade chapit la Kopi




Yoane 16:2
27 Referans Kwoze  

Wazazi wake walisema hivi kwa sababu waliogopa wakubwa wa Wayuda. Wakubwa wale walikuwa wamekwisha kupatana kwamba mutu yeyote anayesadiki kuwa Yesu ndiye Kristo, atatengwa asiingie katika nyumba ya kuabudia.


Musiwaogope wale wanaoweza kuua tu mwili, lakini wasioweza kuua roho. Lakini zaidi mumwogope Mungu anayeweza kuharibu mwili pamoja na roho katika jehenamu.


Wakati Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa tano, nikaona chini ya mazabahu, roho za watu waliouawa kwa sababu ya kutangaza Neno la Mungu na kwa sababu ya ushuhuda wao.


Hata hivi wengi kati ya wakubwa wa Wayuda wakamwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Wafarisayo, hawakushuhudia kwamba wameamini. Waliogopa kwamba watatengwa wasiingie katika nyumba ya kuabudia.


“Heri ninyi wakati watu wanapowachukia, wanapojitenga nanyi, wanapowatukana na kuchafua jina lenu kwa ajili ya Mwana wa Mutu!


Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!


wakati tunaposingiziwa, tunajibu kwa upole. Hata sasa tunahesabiwa kama takataka za dunia, na kila mutu anatuangalia kama uchafu.


Naye Stefano akasema: “Ninaona mbingu zimefunguliwa wazi, naye Mwana wa Mutu akisimama na mamlaka karibu na Mungu.”


“Halafu watu watawatoa kusudi muteswe na kuuawa, na watu wa mataifa yote watawachukia ninyi kwa ajili yangu.


Wakamujibu: “Wewe, uko mwenye zambi kabisa tangu kuzaliwa kwako! Unataka kutufundisha?” Halafu wakamufukuza inje.


Wanawaambia wale wanaokutana nao hivi: Muikae mbali nami; musinikaribie kwa sababu mimi ni mutakatifu! Watu hao wananikasirikisha sana, hasira yangu ni kama moto usiozimika.


Wajumbe wa lile Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kutaka kuwaua mitume.


Yesu akamwambia: “Ee mama, unisadiki; kutakuwa wakati hamutamwabudu Baba juu ya mulima huu wala Yerusalema.


nilikuwa na bidii sana hata nilitesa kanisa. Kuelekea mambo ya kuhesabiwa kwa njia ya kushika Sheria, mimi sikupatikana na kosa lo lote.


Wenye hekima kati ya watu watawafundisha wengi. Hata hivyo, kwa siku chache watauawa kwa upanga au kwa moto, watakamatwa mateka au kunyanganywa mali zao.


Lakini kutakuwa wakati, nao umekwisha kutimia, wale wanaoabudu kwa kweli watakapomwabudu Baba katika roho na ukweli; kwa maana Baba anataka watu wanaoabudu kwa namna ile.


“Nimewaambia ninyi maneno hayo kwa mifano. Lakini kutakuwa wakati sitasema nanyi tena kwa mifano, lakini nitawaambia ninyi waziwazi juu ya Baba.


Kutakuwa wakati, nao umetimia, ndio wakati mutakaposambazwa, kila mutu akijiendea ngambo yake mwenyewe, nanyi mutaniacha peke yangu. Lakini mimi si peke yangu kabisa, kwa sababu Baba yuko pamoja nami.


Wakaaji wa muji wakamwendea Yoasi, wakamwambia: “Umutoe mwana wako tumwue, maana ameharibu mazabahu ya mungu Bali na kuivunja sanamu ya mungu Ashera iliyokuwa karibu nayo.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite