Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 15:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Lakini watawafanyia ninyi haya yote kwa ajili yangu, kwa sababu hawamujui yule aliyenituma.

Gade chapit la Kopi




Yoane 15:21
35 Referans Kwoze  

Na watu wote watawachukia kwa ajili yangu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ataokolewa.


Watafanya hivi kwa sababu hawakumujua Baba wala mimi.


Basi wakamwuliza: “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu: “Hamunijui mimi wala hamumujui Baba yangu. Kama mungenijua mimi, mungemujua Baba yangu vilevile.”


“Halafu watu watawatoa kusudi muteswe na kuuawa, na watu wa mataifa yote watawachukia ninyi kwa ajili yangu.


Vilevile mutapelekwa mbele ya wakubwa na wafalme kwa ajili yangu, kusudi mutoe ushuhuda wangu mbele yao na mbele ya watu wa mataifa mengine.


Basi mitume wakatoka katika baraza, wakifurahi sana kwa sababu walistahili kuzarauliwa kwa kuteswa kwa ajili ya Yesu.


Wewe ni muvumilivu; umeteswa kwa ajili ya jina langu, lakini haukuregea.


katikati ya ndimi za moto kwa kuazibu wale wanaokataa kumujua Mungu na wale wasiokubali Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.


Mugeuze mafikiri, murudie katika usawa, muache kufanya zambi. Ninasema neno hili kwa kuwapatisha haya, kwa sababu wamoja kati yenu hawamujui Mungu.


Hakuna hata mutawala mumoja kati ya watawala wa dunia hii aliyeelewa hekima ile. Kama wangeielewa wasingemutundika Bwana wa utukufu juu ya musalaba.


Hivi kufuatana na vile walivyokataa kumutambua Mungu, Mungu akawaacha wafuate akili yao ya upotevu, kusudi wafanye mambo wasiyopaswa kufanya.


Kwa maana nilipokuwa nikipitapita katika muji wenu nilichunguza nafasi zenu za kuabudia, nikaona hata mazabahu mamoja ambako waliyochora maandiko haya: ‘Kwa ajili ya mungu asiyejulikana.’ Basi yule munayemwabudu pasipo kumujua ndiye mimi ninayemuhubiri kwenu sasa.


Nami nitamwonyesha mateso ya namna gani atakayopaswa kupata kwa ajili yangu.”


“Sasa wandugu zangu, ninajua kwamba ninyi na wakubwa wenu mumemutendea Yesu hayo yote pasipo kujua nini munayofanya.


Yesu akajibu: “Kama nikijitafutia sifa yangu mwenyewe, sifa ile haina maana. Baba yangu ndiye anayenisifu, yule munayejidai kwamba ni Mungu wenu!


“Heri ninyi wakati watu wanapowachukia, wanapojitenga nanyi, wanapowatukana na kuchafua jina lenu kwa ajili ya Mwana wa Mutu!


Kwa maana mutu anayetaka kulinda uzima wake, ataupoteza; lakini yule atakayetoa uzima wake kwa ajili yangu, ataupata tena.


Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!


Wanaokutumainia wasifezeheke kwa sababu yangu, ee Bwana wetu, Yawe wa majeshi; wanaokutafuta, wasizarauliwe kwa sababu yangu, ee Mungu wa Israeli.


“Heri ninyi, wakati watu wanapowatukana na kuwatesa na kuwasingizia kila namna ya ubaya kwa sababu yangu.


Na watu wote watawachukia kwa ajili yangu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho, ataokolewa.


Lakini mbele mambo hayo yote yatokee, mutakamatwa na kuteswa. Watawapeleka kwenda kuhukumiwa katika nyumba za kuabudia na kuwatia katika vifungo. Vilevile mutapelekwa mbele ya wafalme na ya wakubwa kwa ajili ya jina langu,


Watu wote watawachukia kwa ajili ya jina langu.


Ninyi hamumujui, lakini mimi ninamujua. Kama ningesema kwamba simujui, ningekuwa mwongo kama ninyi. Lakini ninamujua na ninashika neno lake.


Kama nisingetenda kati yao matendo yasiyofanywa na mutu mwingine, wasingekuwa na zambi. Lakini sasa wameyaona lakini hata hivi wananichukia mimi pamoja na Baba yangu.


Baba mwenye haki, ijapokuwa dunia haikujui, mimi ninakujua na hawa wanajua kwamba ulinituma.


Lakini kwa kuzuiza habari za jambo lililotokea zisisambae zaidi kati ya watu, tuwakataze kwa ukali wasiendelee tena kusema na mutu yeyote wakitaja jina la Yesu.”


Na hata huku yuko na mamlaka aliyopewa na wakubwa wa makuhani kusudi afunge wote wanaoomba kwa jina lako.”


“Kweli mimi mwenyewe niliwaza kwamba nilipaswa kufanya yote ninayoweza kwa kupinga jina la Yesu wa Nazareti.


Muangalie namna Baba alivyoonyesha upendo wake kwetu hata tupate kuitwa watoto wa Mungu! Na kwa hakika sisi ndio wao! Ndiyo maana watu wa dunia hawatutambui, kwa sababu hawakumujua Mungu.


Kwa maana hawa walianza safari yao kwa ajili ya kazi ya Kristo bila kupokea musaada wowote toka kwa watu wasioamini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite