Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 15:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.

Gade chapit la Kopi




Yoane 15:14
19 Referans Kwoze  

Kwa maana yeyote anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa katika mbingu, huyu ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu.”


Kwa maana kumupenda Mungu ni kutii amri zake. Na amri zake si ngumu,


Na maandiko haya yakatimia: “Abrahamu alimwamini Mungu na kwa hiyo akahesabiwa kuwa mwenye haki.” Na Mungu akamwita rafiki yake.


“Anayekubali amri zangu na kuzitii, ni yeye anayenipenda. Baba yangu atamupenda yule anayenipenda, na mimi nitamupenda vilevile na nitajitambulisha kwake.”


“Kama munanipenda, mutashika amri zangu.


“Ninawaambia ninyi warafiki zangu: musiwaogope wale wanaoua mwili tu lakini hawawezi kufanya kitu kingine zaidi.


Sasa kwa kuona munajua jambo hili, mutakuwa wenye heri kama mukilifanya.


Sikiliza ewe Israeli, mutumishi wangu, wewe, Yakobo ambaye nimekuchagua, wewe wa uzao wa Abrahamu, rafiki yangu;


Halafu mama yake akawaambia watumishi: “Mufanye kila kitu atakachowaambia.”


Mumesikia jinsi nilivyowaambia kwamba ninajiendea, lakini nitawarudilia tena. Kama mungenipenda, mungefurahia kujua kwamba ninakwenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mukubwa kuliko mimi.


Si wewe, ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa inchi hii wakati watu wako Waisraeli walipoingia katika inchi hii, ukawapa wazao wa Abrahamu rafiki yako, ikuwe yao milele?


Ninaingia katika bustani yangu, dada yangu, muchumba wangu. Ninakusanya manemane na majani yenye harufu, ninakula sega langu la asali, ninakunywa divai yangu na maziwa yangu. Mukule, enyi warafiki, mukunywe; mukunywe sana, wapendwa wangu.


Warafiki wengi wanaweza kumwangusha mutu, lakini kuna rafiki mwaminifu kuliko ndugu.


Basi, Musa na Haruni wakafanya hivyo. Hakika, walifanya kama vile Yawe alivyowaamuru.


Kwa hiyo, Ruta akakwenda kule katika kiwanja cha kupepetea, akafanya jinsi mama mukwe wake alivyomwamuru.


Yeye hakumwasi Yawe wala hakuacha kumufuata, lakini alishika amri ambazo Yawe alimupa Musa.


Nao walifika, wakaitwaa na kuirizi. Lakini wao hawakukusikiliza, wala hawakufuata sheria zako. Hawakutenda mambo uliyoamuru. Ndiyo maana utawafanya wapatwe na hasara hii.


Basi, nikafanya kama nilivyoamriwa. Siku hiyo, wakati wa muchana, nikafunga muzigo wangu kama muzigo wa mutu anayekimbia. Magaribi nikatoboa ukuta na giza lilipokuwa likiingia, nikatoka, nikibeba muzigo wangu juu ya mabega, watu wote wakiniona.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite