Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 15:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 “Nimewaambia ninyi maneno haya kusudi mufurahi sawa mimi, na furaha yenu ikuwe kubwa kabisa.

Gade chapit la Kopi




Yoane 15:11
21 Referans Kwoze  

Basi, Mungu anayekuwa musingi wa matumaini, awajaze furaha kamili na amani kutokana na imani yenu; hata tumaini lenu lipate kuongezeka kwa nguvu ya Roho Mutakatifu.


Lakini sasa ninarudi kwako, nami ninasema maneno haya nikingali katika dunia, kusudi furaha yangu kubwa kabisa ikuwe ndani yao.


Mpaka sasa hamujaomba kitu kwa jina langu. Muombe, nanyi mutapewa, na furaha yenu itakuwa kubwa kabisa.


Tunawaandikia ninyi maneno haya kusudi tupate kujazwa na furaha kabisa.


Ninyi munamupenda ijapokuwa hamujamwona, na munamwamini ijapokuwa sasa hamumwoni. Na zaidi ya ile munashangilia kwa furaha isiyoweza kuelezwa, inayojaa utukufu,


Nina maneno mengi ya kuwaambia, lakini sitaki kuyaandika ndani ya barua. Ninatumaini nitawatembelea na kusemezana pamoja nanyi uso kwa uso, kusudi tupate kujazwa na furaha kabisa.


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Hatutafuti kuwaamuru ninyi juu ya mambo yale munayopaswa kuamini, maana munasimama imara katika imani. Lakini tunataka kutumika pamoja nanyi kusudi mupate kufurahi.


Mukuwe na furaha siku zote.


Kwa hivi ilitupasa kushangilia na kufurahi, kwa maana mudogo wako huyu alikuwa amekufa na amefufuka, alikuwa amepotea na sasa ameonekana.’ ”


Anapokipata atawaita warafiki na jirani zake na kuwaambia: ‘Mufurahi pamoja nami kwa sababu nimepata kikoroti kile cha feza nilichokipoteza!’


Basi niko na uhakika juu ya jambo hili nami ninajua kwamba nitabaki. Nitakaa pamoja nanyi kwa kuwasaidia kusudi mupate kuendelea na kuwa na furaha katika imani.


Musilewe divai kwa maana inaleta upotovu, lakini mujazwe na Roho.


Mwenye bibi arusi ndiye bwana-arusi; lakini rafiki ya bwana arusi anasimama karibu naye na kumusikiliza, anafurahi sana kusikia sauti ya bwana-arusi. Na ni hivi mimi ninafurahi, na furaha yangu imetimia sasa.


Atakapomwona, atamubeba kwa furaha juu ya mabega.


Kisha, mulete yule ngombe mwenye kunona na kumuchinja; nasi tutakula na kufurahi pamoja.


Nitafurahi kuwatendea mema; nitawasimika siku zote katika inchi hii na kuwatendea kwa uaminifu.


Mungu anasema: Kisha kutaabika sana, mutumishi wangu atafurahi. Kwa njia ya kujulikana kwa huyo mutumishi wangu wa haki, atawafanya wengi wakuwe wenye haki, naye atazibeba zambi zao.


Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


Hautaitwa tena: Aliyeachwa, wala inchi yako haitaitwa: “Ukiwa”. Lakini utaitwa: “Ninamufurahia”, na inchi yako itaitwa: “Aliyeolewa”. Maana Yawe amependezwa nawe, naye atakuwa kama mume wa inchi yako.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite