8 Filipo akamwambia: “Bwana, utuonyeshe Baba, na ile itatutoshelea.”
“Nimewaambia ninyi maneno hayo kwa mifano. Lakini kutakuwa wakati sitasema nanyi tena kwa mifano, lakini nitawaambia ninyi waziwazi juu ya Baba.
Lakini mimi nitauona uso wako, maana mimi ni mutu wa haki; nitakapoamuka nitajaa furaha kwa sababu unanitokea.
Kisha atamwomba Mungu na kukubaliwa, atakuja mbele yake kwa furaha, na Mungu atamurudishia utukufu wake.
Heri wale wanaokuwa na moyo safi, maana watamwona Mungu!
Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu. Moyo wangu unakutafuta, roho yangu inasikia kiu yako, ninasikia kiu yako kama inchi inayokauka kwa ukosefu wa maji.
Natanaeli akamwuliza: “Unanijua namna gani?” Yesu akamujibu: “Filipo alipokuwa hajakuita, nilikuona wakati ulipokuwa chini ya muti wa matunda ya tini.”