Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 14:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Yesu akamujibu: “Anayenipenda, atashika maneno yangu. Baba yangu atamupenda, naye Baba pamoja nami tutaingia ndani yake na kukaa ndani yake.

Gade chapit la Kopi




Yoane 14:23
30 Referans Kwoze  

“Anayekubali amri zangu na kuzitii, ni yeye anayenipenda. Baba yangu atamupenda yule anayenipenda, na mimi nitamupenda vilevile na nitajitambulisha kwake.”


“Kama munanipenda, mutashika amri zangu.


Kwa hiyo muchunge ndani ya mioyo yenu mafundisho muliyosikia tangia mbele. Kama mukichunga mafundisho yale muliyosikia tangia mbele, mutakaa ndani ya Mwana pamoja na Baba.


Lakini ninyi, watoto wangu, muko watoto wa Mungu, nanyi mumewashinda manabii wa uongo; maana roho anayekaa ndani yenu ni mwenye uwezo kuliko yule anayekaa ndani ya watu wa dunia.


Kuna ulinganisho gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi ni hekalu la Mungu Mwenye Uzima kama vile yeye mwenyewe alivyosema: “Nitakaa na kuishi pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”


Ukikaa chini ya ulinzi wa Mungu Mukubwa, ukiishi chini ya kivuli cha Mungu Mwenye Nguvu,


Mimi na Baba yangu tuko mumoja.”


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anakaa ndani yangu, nami ninakaa ndani yake.


naye ndiye Roho wa ukweli. Dunia haiwezi kumupokea, kwa sababu haimwoni wala haimujui. Lakini munamujua, kwa maana anaishi pamoja nanyi naye anakuwa ndani yenu.


Kisha Mungu akasema: “Tumufanye mutu kwa mufano wetu, anayefanana nasi, atawale samaki wa bahari, ndege wa anga, nyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vinavyotambaa.”


Sikuona hekalu ndani ya muji ule, maana Bwana wetu Mungu Mwenye Uwezo na yule Mwana-Kondoo ndio hekalu lake.


Basi, tushuke chini na kuvuruga luga yao kusudi wasielewane wao kwa wao.”


Hakutakuwa tena kitu chochote kinacholaaniwa na Mungu. Kiti cha kifalme cha Mungu na cha Mwana-Kondoo kitakuwa ndani ya muji ule, na watumishi wa Mungu watamwabudu.


Maombi ya Musa, mutu wa Mungu. Ee Bwana, tangia vizazi vyote, wewe umekuwa usalama wetu.


Kweli, kweli ninawaambia: kama mutu akishika maneno yangu, hatakufa hata milele.”


Halafu Wayuda wakamwambia: “Sasa tunajua hakika kwamba uko na pepo! Abrahamu amekufa, na manabii wamekufa vilevile, nawe unasema kwamba mutu akishika maneno yako, hatakufa hata milele.


Asiyenipenda hashiki maneno yangu. Na neno munalosikia nikisema halitoki kwangu, lakini linatoka kwa Baba yangu aliyenituma.


Kama mukishika amri zangu, mutakaa katika upendo wangu, kama vile mimi nilivyoshika amri za Baba yangu na kukaa katika upendo wake.


kwa maana Baba mwenyewe anawapenda. Anawapenda ninyi kwa sababu mumenipenda na kuamini kwamba nilitoka kwa Mungu.


Hivi Kristo apate kukaa ndani ya mioyo yenu kwa njia ya imani, nanyi mupate kuwa na mizizi na musingi katika upendo.


Lakini yule anayetii neno la Mungu yuko na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hili ndilo jambo linalotuonyesha kwamba sisi tunaungana na Mungu:


Kwa maana kumupenda Mungu ni kutii amri zake. Na amri zake si ngumu,


Na upendo ni kuishi katika kutii amri za Mungu. Hii ndiyo ile amri muliyoisikia tangu mwanzo: muishi katika upendo.


Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite