Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 14:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Nami nitafanya chochote mutakachoomba kwa jina langu, kusudi Baba atukuzwe kwa njia ya Mwana.

Gade chapit la Kopi




Yoane 14:13
36 Referans Kwoze  

Kama mukikaa ndani yangu na maneno yangu yanakaa ndani yenu, mutaomba chochote munachotaka, nanyi mutakipewa.


Ni kwa hiyo ninawaambia kwamba munapoomba kwa ajili ya hitaji la kitu fulani, mwamini kama mumekwisha kukipokea, na kwa njia hiyo mutakipewa.


Na kitu chochote mutakachoomba, mukiamini, mutakipata.”


“Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.


Nasi tuko na tumaini hili mbele ya Mungu: tunajua kwamba atatusikiliza tukimwomba kitu chochote kufuatana na mapenzi yake.


“Siku ile itakapotimia, ninyi hamutaniuliza juu ya kitu fulani. Kweli, kweli ninawaambia: Baba atawapa chochote mutakachomwomba kwa jina langu.


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


Ninyi hamukunichagua mimi, lakini ni mimi niliyewachagua ninyi. Nami nimewatuma muende kuzaa matunda yasiyokuwa na mwisho. Kwa hiyo Baba atawapa chochote munachoomba kwa jina langu.


Kama mukiomba kitu chochote kwa jina langu, nitakifanya.


Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa.


Ninaweza vyote kwa njia ya Kristo anayenitia nguvu.


Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.


Na katika kuungana kwetu na Yesu Kristo na kwa njia ya kumwamini tunapata uhuru wa kufika mbele ya Mungu tukiwa na tumaini kubwa.


Siku ile itakapotimia, mutamwomba Baba kwa jina langu. Mimi sisemi kwamba nitawaombea ninyi kwa Baba,


Mimi na Baba yangu tuko mumoja.”


Kwa maana, kwa njia ya Kristo sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, tumefunguliwa njia ya kufika mbele ya Baba katika Roho mumoja.


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Siku ya mwisho ya sikukuu ile iliyokuwa siku kubwa, Yesu akasimama na kusema hivi kwa sauti: “Mutu akiwa na kiu, akuje kwangu akunywe.


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


Halafu Yesu akasema hivi kwa sauti: “Anayeniamini haniamini mimi tu, lakini anamwamini vilevile yule aliyenituma.


Nami ninawaambia: muombe nanyi mutapewa; mutafute nanyi mutapata; mupige hodi nanyi mutafunguliwa mulango.


Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.


Basi Yesu akaongeza kuwaambia Wayuda: “Kweli, kweli, ninawaambia: Mwana hawezi kufanya kitu kwa mafikiri yake mwenyewe; anafanya tu kile ambacho anaona Baba akifanya. Na mambo yote Baba anayofanya, Mwana anayafanya vilevile.


Basi kwa njia ya Yesu, tumutolee Mungu sadaka za kumusifu siku zote, maana yake kutangaza kwamba tunaaminia jina lake.


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


Kwa sababu hiyo ninapiga magoti mbele ya Baba Mungu,


lakini yeyote atakayekunywa maji yale nitakayomupa, hatasikia kiu tena hata kidogo. Maji nitakayomupa yatakuwa ndani yake kama chemichemi inayotiririka maji ya uzima wa milele.”


Yesu akamujibu: “Kama ungejua kitu Mungu anachoweza kukupatia, na ni nani anayekuomba maji ya kunywa, wewe ndiwe ungemwomba, naye angekupa maji ya uzima.”


Lakini mimi ninawaambia ukweli: ni faida kwenu mimi niende, kwa maana nisipokwenda, Musaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, nitamutuma kwenu.


Wakati Yuda alipokwisha kutoka, Yesu akasema: “Sasa Mwana wa Mutu ametukuzwa, na Mungu ametukuzwa kwa njia yake.


Kwa hiyo yule anayesema kwa luga ya ajabu, aombe Mungu amupatie uwezo wa kuitafsiri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite