Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 13:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kisha akatia maji ndani ya bakuli, na kuanza kunawisha miguu ya wanafunzi wake na kuipanguza na kile kitambaa alichokifunga katika kiuno.

Gade chapit la Kopi




Yoane 13:5
30 Referans Kwoze  

Halafu akamugeukia yule mwanamuke na kumwambia Simoni: “Unamwona mwanamuke huyu? Niliingia ndani ya nyumba yako, nawe haukunipa maji ya kunawa miguu yangu, lakini mwanamuke huyu amenawa miguu yangu na machozi yake na kuipanguza na nywele zake.


Akasema: “Bwana zangu, karibu katika nyumba yangu mimi mutumishi wenu. Munaweza kunawa miguu na kulala kwangu usiku wa leo. Asubui mapema mutaweza kuendelea na safari yenu.” Lakini, wao wakasema: “Hapana! Sisi tutalala huku katika barabara.”


Sherti ajulikane kwa matendo yake mema. Anapaswa kuwa mutu aliyeadibisha watoto wake vizuri, aliyekaribisha wageni, aliyewapokea watu wa Mungu akiwanawisha miguu, aliyewasaidia wenye taabu na aliyejitolea kwa kutenda mema ya kila namna.


Mutaletewa maji kidogo kusudi munawe miguu na kupumzika chini ya muti.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


Basi tumwendee Mungu kwa moyo wa uaminifu, kwa imani kamilifu, kwa moyo uliosafishwa toka zamiri mbaya na mwili uliosafishwa na maji safi.


Alifanya hivi kusudi atakase kanisa kwa ajili ya Mungu, akilisafisha kwa maji na kwa neno.


Na wamoja kati yenu walikuwa kama wao. Lakini mumesafishwa toka zambi, mumetakaswa na kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.


Basi sasa, unangojea nini? Simama ubatizwe na kuondolewa zambi zako, ukiomba kwa jina la Bwana.’ ”


Mufalme Yosafati akauliza: “Hakuna nabii yeyote hapa wa Yawe ambaye tunaweza kumwuliza shauri la Yawe?” Mutumishi mumoja wa mufalme Yoramu wa Israeli akajibu: “Elisha mwana wa Safati iko hapa. Yeye alikuwa mutumishi wa Elia.”


Abigaili alisimama, na kuinama mbele yao uso mpaka chini, akasema: “Mimi ni mujakazi tu. Niko tayari kunawisha miguu ya watumishi wa bwana wangu.”


Huyo mutu atafua nguo zake, atanyoa nywele zake, na kuoga, naye atakuwa safi. Nyuma ya hayo atarudi ndani ya kambi, lakini atakaa inje ya hema lake kwa muda wa siku saba.


Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji ya ubatizo wake na kwa damu ya kufa kwake. Hakukuja na maji tu, lakini pamoja na maji na damu. Naye Roho ndiye anayeshuhudia mambo yale kwa sababu Roho ni wa ukweli.


Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.


Lakini askari mumoja akamuchoma mukuki katika ubavu; mara moja damu na maji vikatoka.


Akakuja kuinama kwenye miguu ya Yesu, akilia. Machozi yake yakamwangika juu ya miguu ya Yesu, akaipanguza na nywele zake, akaibusu na kuipakaa marasi.


Siku hiyo, kutatokea chemichemi ya kutakasa zambi na uchafu wa wazao wa Daudi na wakaaji wote wa Yerusalema.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


Mujisafishe, mujitakase; muondoe matendo yenu maovu mbele yangu. Muache kutenda mabaya,


Kisha uwapeleke Haruni na wana wake kwenye mulango wa hema la mukutano na kuwanawisha.


Yesu akamwambia: “Aliyekwisha kuoga hahitaji kunawa tena, isipokuwa miguu yake tu, kwa maana mwili wake wote ni safi. Na ninyi ni safi, lakini si wote.”


Petro akamwambia: “Hautanawisha miguu yangu hata kidogo!” Yesu akamujibu: “Nisipokunawisha miguu, hauna ushirika pamoja nami.”


Yule musimamizi alipowakaribisha ndani ya nyumba kwa Yosefu, akawapa maji ya kunawa miguu yao, na punda wao akawakulisha.


Hivyo akawapeleka katika nyumba yake na kuwapa punda wao malisho. Hao wasafiri wakanawa miguu yao, wakakula na kunywa.


Alipofika kwenye Simoni Petro, Petro akamwambia: “Bwana, ni kweli wewe utaninawisha miguu?”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite