35 Watu wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, ikiwa munapendana ninyi kwa ninyi.”
Yule anayemupenda ndugu yake, anaishi katika mwangaza na ndani yake hamuna kitu kinachoweza kuangusha mwingine katika zambi.
Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.
Lakini yule anayetii neno la Mungu yuko na upendo kamili wa Mungu ndani yake. Hili ndilo jambo linalotuonyesha kwamba sisi tunaungana na Mungu:
Na sasa Mama, ninakusihi: tupendane. Basi hii si amri mupya ninayokuandikia, lakini ni amri ile tuliyopokea tangu mwanzo.