Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 13:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yesu akamwambia: “Aliyekwisha kuoga hahitaji kunawa tena, isipokuwa miguu yake tu, kwa maana mwili wake wote ni safi. Na ninyi ni safi, lakini si wote.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 13:10
23 Referans Kwoze  

Ninyi mumekwisha kuwa safi kwa kuwa mumeshika maneno niliyowaambia.


Basi mutu yeyote anapoungana na Kristo, yeye anakuwa kiumbe kipya. Mambo ya zamani yametoweka, na sasa hali mupya imefika.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Yule mutu atakayewateketeza atafua nguo zake na kuoga, ndipo atakapoweza kuingia katika kambi.


Yule mutu aliyepeleka yule beberu kwa Azazeli kwanza atafua nguo zake na kuoga ndipo atakapoweza kuingia ndani ya kambi.


Sisi wote tunakosa kwa njia mbalimbali. Mutu asiyekosa katika masemi yake, huyo ni mutu mukamilifu, naye yuko na uwezo wa kutawala mwili wake wote.


Hizo ni kanuni za kimutu zinazoelekea vyakula na vinywaji pamoja na desturi mbalimbali za utakaso za kidini. Nazo zinaamuriwa kushikwa mpaka upate kutimia wakati wa kutengeneza vitu vyote upya.


Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa, alinde uzima wenu wote ndiyo roho, moyo na mwili wenu, kusudi visikutiwe na kosa wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakaporudia.


Utusamehe makosa yetu, kama sisi tunavyowasamehe wanaotukosea,


Siku hizo na wakati huo, uovu utatafutiwa katika inchi ya Israeli, lakini hautapatikana; zambi itatafutiwa katika inchi ya Yuda, lakini haitapatikana; maana mimi nitawasamehe wale ambao nimewaponyesha. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wewe ni nzuri kabisa, ee mupenzi wangu, wewe hauna kilema chochote.


Hakika, hakuna mutu wa haki katika dunia anayetenda vizuri siku zote bila kutenda zambi.


Simoni Petro akamwambia tena: “Basi Bwana, ikiwa ni vile usininawishe miguu tu, lakini uninawishe mikono na kichwa vilevile.”


“Sisemi juu ya ninyi wote; ninawajua wale niliowachagua. Lakini inafaa maneno haya yanayosemwa na Maandiko Matakatifu yatimie: ‘Yule aliyechangia chakula nami, amenigeuka.’


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite