Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 13:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kulikuwa kumebaki siku moja mbele ya kutimia kwa sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua kwamba saa yake ya kutoka katika dunia na kurudi kwa Baba yake imetimia. Yeye alikuwa akiwapenda watu wake waliokuwa katika dunia, na akaendelea kuwapenda mpaka mwisho.

Gade chapit la Kopi




Yoane 13:1
44 Referans Kwoze  

Yesu akawajibu: “Saa ya kutukuzwa kwa Mwana wa Mutu imetimia.


Sisi tuko na upendo kwa sababu Mungu ndiye aliyetupenda wa kwanza.


Ninawapa amri mupya: mupendane ninyi kwa ninyi. Kama mimi nilivyowapenda, nanyi mupendane vilevile.


Nilitoka kwa Baba, nami nimekuja katika dunia. Sasa ninaacha dunia na kurudi kwa Baba.”


Yesu alijua kwamba Baba yake ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, na kwamba yeye mwenyewe alitoka kwa Mungu na anarudi kwa Mungu.


Basi Yesu akiwa mwenye kujua maneno yote yatakayomupata, akawaendea na kuwauliza: “Munamutafuta nani?”


Ni yeye atakayewasimamisha ninyi imara mpaka mwisho kusudi musishitakiwe juu ya kosa lolote Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo.


Wao si wa dunia, kama vile mimi nisivyokuwa wa dunia.


Wakati Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akainua macho mbinguni na kusema: “Baba, wakati umetimia. Uonyeshe utukufu wa Mwana wako, kusudi Mwana wako aonyeshe utukufu wako vilevile.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.


Na sasa, Baba, unipe utukufu karibu nawe, utukufu unaokuwa sawa na ule niliokuwa nao pamoja nawe mbele ya kuumbwa kwa dunia.


Kisha akarudi kwenye wanafunzi wake na kuwaambia: “Mungali munalala na kupumzika? Angalia, saa imetimia, sasa Mwana wa Mutu anatolewa katika mikono ya wenye zambi.


Kwa sababu hiyo, mukuwe tayari kwa kutumikisha akili yenu. Mukeshe na muweke tumaini lenu lote katika baraka ile mutakayopewa wakati Yesu atakapotokea.


Lakini tunatamani sana kwamba kila mumoja kati yenu aendelee kuonyesha bidii ile mpaka mwisho, kusudi mambo yale munayotumainia yapate kutimizwa.


Lakini Kristo ni mwaminifu kama Mwana anayesimamia nyumba ya Mungu. Na sisi ndio nyumba ile, kama tukiendelea kuwa na uhodari na kuaminia kupata mambo tunayotumainia.


Lakini katika mambo haya yote tunapata ushindi kabisa kwa njia ya yule aliyetupenda.


Nimekujulisha kwao, na nitaendelea kukujulisha kusudi upendo ule unaokuwa nao kwangu ukuwe ndani yao, nami mwenyewe nikuwe ndani yao.”


Mumesikia jinsi nilivyowaambia kwamba ninajiendea, lakini nitawarudilia tena. Kama mungenipenda, mungefurahia kujua kwamba ninakwenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mukubwa kuliko mimi.


Sikukuu ya Wayuda ya Pasaka ilikuwa karibu. Basi watu wengi toka katika vijiji wakaenda Yerusalema kusudi wajitakase mbele ya Pasaka.


Basi wakatafuta kumufunga, lakini hakuna mutu aliyemukamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijatimia.


Na Yesu akawaambia: “Wakati unaofaa kwangu haujatimia; lakini wakati wowote unafaa kwenu.


Na Pasaka, ambayo ni moja ya sikukuu za Wayuda, ilikuwa karibu.


Siku zote nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu, ninyi hamukunikamata. Lakini hii ni saa yenu; saa ya utawala wa bwana wa giza.”


Siku za Yesu za kunyanyuliwa mbinguni zikakaribia. Kwa hiyo akakusudia sana kwenda Yerusalema,


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


mimi Yawe nilimutokea kwa mbali. Nami nimekupenda kwa mapendo ya milele, kwa hiyo nimeendelea kuwa mwema kwako.


Yesu alisema maneno haya wakati alipokuwa akifundisha katika hekalu, kwenye sanduku za kuwekea matoleo. Hakuna mutu aliyemufunga, kwa sababu wakati wake ulikuwa haujatimia.


nikifurahia dunia na wakaaji wake, na kupendezwa kuwa pamoja na wanadamu.


Wakati sikukuu ya Pasaka ya Wayuda ilipokaribia, Yesu akaenda Yerusalema.


Wamoja walizani kama Yesu amemwambia aende kununua vitu walivyohitaji kwa sikukuu, au aende kuwasaidia wamasikini, kwa sababu Yuda ndiye aliyekuwa akichunga mufuko wa feza.)


lakini sherti dunia ijue kama ninamupenda Baba, nami ninafanya kama alivyoniagiza. “Musimame, tutoke hapa.


Kisha, Yesu akiwa anajua kwamba mambo yote yametimia, akasema hivi kusudi Maandiko Matakatifu yatimie: “Ninasikia kiu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite