Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 12:47 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

47 Mutu akisikia maneno yangu pasipo kuyashika, si mimi nitakayemuhukumu. Kwa maana sikukuja kuhukumu dunia, lakini nilikuja kuiokoa.

Gade chapit la Kopi




Yoane 12:47
13 Referans Kwoze  

Mungu hakumutuma Mwana wake katika ulimwengu kusudi ahukumu ulimwengu, lakini kusudi ulimwengu uokolewe naye.


Yule anayenikataa na asiyekubali maneno yangu atahukumiwa kufuatana nayo. Ni lile neno nililosema ndilo litakalomuhukumu siku ya mwisho.


Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


Kwa maana Mwana wa Mutu alikuja kutafuta na kuokoa yule aliyepotea.”


Musizanie kwamba mimi nitawashitaki kwa Baba. Atakayewashitaki ninyi ni Musa, ambaye mulimutumainia.


Kwa maana Mwana wa Mutu hakukuja kutumikiwa, lakini kutumikiana na kutoa maisha yake kusudi awakomboe watu wengi.”


Mutambue kwamba njia ya kuvumilia kwa Bwana wetu ni wakati muzuri anaowapatia kusudi mupate kuokolewa. Na hiyo ni kufuatana na vile ndugu yetu mupendwa Paulo alivyowaandikia akiongozwa na hekima aliyopewa na Mungu.


Nina maneno mengi ya kusema juu yenu na ya kuwahukumu. Lakini yule aliyenituma ni wa kweli, nami ninajulisha dunia maneno yale niliyosikia kwake.”


“Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [


Kisha wakaondoka kwenda katika kijiji kingine.


Kwa maana Mwana wa Mutu alikuja kuokoa yule aliyepotea.]


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite