Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 12:43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

43 Wao walipenda kusifiwa na watu kuliko kupata sifa inayotoka kwa Mungu.

Gade chapit la Kopi




Yoane 12:43
20 Referans Kwoze  

Basi namna gani mutaweza kuamini, ninyi munaopokea sifa kutoka wamoja kwa wengine, lakini hamutafuti sifa inayotoka kwake anayekuwa Mungu peke yake?


“Mimi sipokei sifa kutoka kwa watu.


Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.


Hatukutafuta sifa ya watu wala yenu, wala ya mutu mwingine yeyote,


Kwa maana, mutu anayekubaliwa si yule anayejisifu mwenyewe, lakini ni yule anayesifiwa na Bwana.


“Basi wakati unapomusaidia masikini, usipige baragumu, kama vile wanafiki wanavyofanya katika nyumba za kuabudia na katika barabara kusudi wasifiwe na watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Kama mutu akitaka kunitumikia, anapaswa kunifuata, na hivi mutumishi wangu atakuwa popote nitakapokuwa. Mutu akinitumikia, Baba yangu atamupa heshima.


Yesu akajibu: “Kama nikijitafutia sifa yangu mwenyewe, sifa ile haina maana. Baba yangu ndiye anayenisifu, yule munayejidai kwamba ni Mungu wenu!


Naye akamwambia: ‘Ni vizuri wewe mutumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, ninakupa utawala juu ya miji kumi.’


Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Lakini mapambo yenu yanapaswa kuwa ya ndani ya moyo yasiyoweza kuharibika. Sherti mapambo yale yakuwe yenye kutokana na roho ya amani na upole inayohesabiwa kuwa ya bei kali mbele ya Mungu.


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Maana Yawe ni mufalme; yeye anatawala mataifa.


Saulo akajibu: “Nimefanya zambi. Hata hivyo, uniheshimishe sasa mbele ya wazee wa watu wangu na Waisraeli. Uniruhusu nirudi pamoja nawe kusudi nimwabudu Yawe, Mungu wako.”


Kuogopa watu ni kujitega mwenyewe, lakini anayemutumainia Yawe yuko salama.


Mutu anayesema kwa mamlaka yake mwenyewe, anajitafutia sifa yake mwenyewe. Lakini yeye anayetafuta sifa ya yule aliyemutuma, huyu ni mwenye ukweli wala hana ubaya wowote.


Lakini Muyuda wa kweli ni yule anayekuwa Muyuda kwa ndani, nako kutahiriwa kwa kweli ni kule Roho Mutakatifu anakofanya ndani ya moyo wa mutu, wala si kule kunakofanyika kwa njia ya maandiko ya Sheria. Mutu wa namna hii hapati sifa kutoka kwa watu lakini kutoka kwa Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite