Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 12:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Lakini mimi, nitakaponyanyuliwa toka katika dunia, nitawavuta watu wote kuja kwangu.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 12:32
23 Referans Kwoze  

Halafu Yesu akawaambia: “Wakati mutakapomunyanyua Mwana wa Mutu juu, mutafahamu kwamba ‘Mimi Ndimi.’ Na zaidi ya hii mutatambua kwamba sifanyi neno lolote kwa mapenzi yangu, lakini ninasema tu yale niliyofundishwa na Baba.


Sawa Musa alivyonyanyua nyoka ya shaba juu ya muti katika jangwa, ni hivi vilevile, sherti Mwana wa Mutu anyanyuliwe,


Kristo yeye mwenyewe alibeba mizigo ya zambi zetu ndani ya mwili wake alipoteswa juu ya musalaba, kusudi tupate kuachana na zambi kabisa na kuishi maisha ya haki. Kwa ajili ya mapigo yake ninyi muliponyeshwa.


Hakuna mutu anayeweza kuja kwangu, isipokuwa anavutwa na Baba aliyenituma, nami nitamufufua siku ya mwisho.


Yeye ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu, wala si kwa ajili ya zambi zetu tu, lakini kwa ajili ya zambi za watu wote.


aliyejitoa mwenyewe kusudi awakomboe watu wote. Na huo ni ushuhuda kwa wakati uliopangwa, kwamba Mungu anataka kuwaokoa watu wake.


Lakini mambo tunayoona ndiyo haya: Yesu alifanywa kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika kusudi kwa neema ya Mungu, Yesu akufe kwa ajili ya watu wote. Na sasa kwa njia ya kile kifo kilichomufikia, amepata utukufu na heshima.


Kristo alitukomboa toka laana ya Sheria, akijitwalia laana hiyo kwa ajili yetu. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu yeyote anayetundikwa juu ya muti amelaaniwa.”


Alikuja kushuhudia ule mwangaza kusudi watu wote wapate kuamini kwa njia yake.


Niliwaongoza kwa huruma, nilishikamana nao kwa upendo; kama baba anavyomunyanyua mutoto mpaka kwenye shavu lake, ndivyo nami nilivyokuwa kwao. Mimi niliinama chini na kuwakulisha.


Nao walikuwa wakiimba wimbo huu mupya wakisema: “Wewe unastahili kukamata kizingo cha karatasi, na kuvunja vifundo vya mihuri yake. Kwa sababu wewe uliuawa, na kwa njia ya damu yako, ulikomboa kwa ajili ya Mungu watu wa kila kabila, wa kila luga, wa kila jamaa na wa kila taifa.


Kufuatana na hiyo, Kristo naye alikufa mara moja tu kwa sababu ya zambi zenu. Yeye alikuwa mwenye haki kwa ajili ya waovu, kusudi awaonyeshe ninyi njia ya kumufuata Mungu. Aliuawa kimwili, lakini kwa uwezo wa Roho Mutakatifu alipata tena uzima.


Yesu akaondoka katika muji akibeba musalaba wake mpaka kwenye nafasi inayoitwa katika Kiebrania “Golgota”, maana yake: “Kilima cha Mufupa wa Kichwa.”


Yeye anasema: Haitoshi tu wewe kuwa mutumishi wangu, kusudi uyainue makabila ya Yakobo, na kurudisha watu wa Israeli waliobaki. Nitakufanya ukuwe mwangaza wa mataifa, kusudi watu wote wapate kuokolewa katika dunia.


Na lile kundi la watu wakamujibu: “Sisi tumesikia katika maandiko ya Sheria kwamba Kristo ataishi milele. Basi namna gani unaweza kusema kama Mwana wa Mutu anapaswa kunyanyuliwa juu? Na huyu Mwana wa Mutu ni nani?”


Unipeleke, tuende haraka, mufalme amenileta katika chumba chake. Tutafurahi na kukushangilia pamoja, tutasifu mapenzi yako kuliko divai. Wabinti wana haki ya kukupenda!


Kisha Abusaloma, akiwa amepanda juu ya nyumbu, alikutana na watumishi wa Daudi. Nyumbu huyo alipokuwa anapita chini ya tawi kubwa la muti wa mwalo, halafu kichwa cha Abusaloma kikakwama kwenye muti wa mwalo. Abusaloma akaachwa akilembelea katika hewa. Lakini nyumbu wake akaendelea mbele.


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


(Ilifanyika hivi kusudi litimie lile neno Yesu alilosema kwa kuonyesha kifo gani atakachokufa.)


Basi, Musa akatengeneza nyoka wa shaba, akamutundika juu ya muti. Kila mutu aliyeumwa na nyoka alipomuangalia nyoka huyo wa shaba, alipona.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite