Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 12:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Kundi la watu waliosimama pale na waliosikia sauti ile wakasema: “Ile ilikuwa ngurumo ya radi!” Wengine wakasema: “Ni malaika aliyekuwa akisema naye!”

Gade chapit la Kopi




Yoane 12:29
12 Referans Kwoze  

Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikinguruma kama uvumi wa maporomoko ya maji mengi na kama ngurumo kubwa ya radi. Sauti ile ilisikilika kama vile sauti ya wapiga vinubi wakati wanapopiga vinubi vyao.


Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.


Kisha yule malaika akatwaa kile chetezo, akakijaza makaa ya moto toka kwenye mazabahu na kukitupa katika dunia. Na halafu kukakuwa ngurumo ya radi, makelele, umeme na tetemeko la inchi.


Kisha nikaona mambo haya: Mwana-Kondoo alipofungua kifundo cha muhuri wa kwanza kati ya ile mihuri saba, nikasikia kimoja kati ya vile viumbe vya ajabu kikisema hivi kwa sauti kama ya ngurumo ya radi: “Kuja!”


Shindo la mabawa ya makerubi iliweza kusikilika hata kwenye kiwanja cha inje, kama sauti ya Yawe wa majeshi anaposema.


Una nguvu kama mimi Mungu? Unaweza kunguruma kwa sauti kama yangu?


Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kusikia sauti ya baragumu juu ya mulima uliokuwa unafuka moshi, wote wakaogopa na kutetemeka. Wote wakasimama mbali,


Basi, siku ya tatu asubui, kukatokea ngurumo na umeme na wingu zito juu ya mulima. Kukasikilika vilevile sauti kubwa ya baragumu ambayo iliwatetemesha watu wote katika kambi.


Nao watu waliosafiri pamoja na Saulo wakasimama na kubaki kimya kwa ajili ya mushangao, kwa maana walisikia sauti lakini hawakuona mutu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite