Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 12:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Siku sita mbele ya Pasaka, Yesu alifika Betania, kwao Lazaro, yule mutu Yesu aliyemufufua.

Gade chapit la Kopi




Yoane 12:1
13 Referans Kwoze  

Kisha Yesu akatoka nao katika muji na kwenda karibu na kijiji cha Betania na pale akainua mikono yake juu na kuwabariki.


Kulikuwa Wagriki wamoja kati ya wale watu waliofika Yerusalema kuabudu wakati wa sikukuu.


Sikukuu ya Wayuda ya Pasaka ilikuwa karibu. Basi watu wengi toka katika vijiji wakaenda Yerusalema kusudi wajitakase mbele ya Pasaka.


Kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Lazaro, muzaliwa wa Betania aliyepatwa na ugonjwa. Wadada zake Maria na Marta walikaa katika kijiji kile.


Kisha akawaacha, akatoka inje ya muji wa Yerusalema, naye akaenda Betania na kulala kule.


Halafu yule marehemu akatoka inje, akiwa amefungwa mikono na miguu kwa vitambaa, na uso wake ukifunikwa na nguo. Yesu akawaambia: “Mumufungue, mumwache ajiendee.”


Yesu akafika Yerusalema na kuingia ndani ya hekalu. Alipokwisha kuangalia vitu vyote pande zote, akaondoka na kwenda Betania pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili, kwa sababu ilikuwa imekwisha kuwa magaribi.


Katika muji ule kulikuwa mwanamuke mumoja aliyejulikana kuwa mwenye mwenendo mubaya. Mwanamuke yule alipopata habari kama Yesu alikuwa akikula ndani ya nyumba ya yule Mufarisayo, akafika akileta chupa la jiwe linalojaa marasi ya bei kali.


Wakati alipokwisha kusema maneno haya, akaita kwa sauti kubwa, akisema: “Lazaro, toka inje.”


Kundi kubwa la Wayuda wakapata habari kwamba Yesu yuko Betania. Kwa hiyo wakaenda kule, si kwa sababu ya Yesu tu, lakini vilevile kwa kumwona Lazaro aliyefufuliwa naye.


Kesho yake lile kundi kubwa la watu waliofika kwa sikukuu ya Pasaka wakasikia kwamba Yesu alikuwa katika njia kuja Yerusalema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite