Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 11:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

39 Yesu akasema: “Muondoshe jiwe hili!” Marta, dada wa yule marehemu, akamujibu: “Bwana, anaanza sasa kunuka, kwa maana ni siku ine sasa tangu alipozikwa!”

Gade chapit la Kopi




Yoane 11:39
11 Referans Kwoze  

Wakati Yesu alipofika, akamukuta Lazaro amekwisha kuzikwa tangu siku ine.


Nao walienda wakiulizana: “Ni nani atakayetusukumia lile jiwe kutoka kwenye kiingilio cha kaburi?”


Watu waovu wanategemea mali zao, wanajisifia wingi wa utajiri wao.


Yeye atabadilisha huu mwili wetu wa uzaifu na kuufananisha na mwili wake wa utukufu kwa nguvu ambayo kwa njia yake anaweza kuwa na mamlaka juu ya vitu vyote.


Kwa jasho la uso wako utajipatia chakula, mpaka utakaporudi katika udongo, maana ulitwaliwa katika udongo. Wewe ni mavumbi na utarudi katika mavumbi.”


maana hautaniachilia kubaki katika kuzimu, hautakubali mutumishi wako mutakatifu apate kuoza.


Hayo ndiyo yanayowapata wanaojitumainia kwa upumbafu, ndio mwisho wa wale wanaojivunia mali zao.


maana malipo ya ukombozi wa maisha ni kubwa sana. Hawezi kutoa kitu chochote kinachotosha,


“Mimi ninaishi kama mugeni kati yenu. Munipatie sehemu ya udongo ya kaburi, kusudi nipate kumuzika marehemu muke wangu.”


Lakini Daudi alipokwisha kutumika sawasawa na kusudi la Mungu katika maisha yake, akakufa na kwenda kukutana na babu zake waliomutangulia, naye akaoza.


Kwa wale wanaopotea ni harufu ya kifo inayoleta kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, ni harufu ya uzima inayoleta uzima. Basi nani anayekuwa na uwezo wa kutimiza kazi ya namna hii?


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite