Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 10:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Basi Yesu akaongeza kusema: “Kweli, kweli ninawaambia: mimi ni mulango wa upango wa kondoo.

Gade chapit la Kopi




Yoane 10:7
12 Referans Kwoze  

Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


Kwa maana, kwa njia ya Kristo sisi wote, Wayuda na watu wa mataifa mengine, tumefunguliwa njia ya kufika mbele ya Baba katika Roho mumoja.


Yesu akasema: “Kweli, kweli ninawaambia: mutu asiyeingia kwa mulango wa upango wa kondoo, lakini anapandia na kuingilia nafasi ingine, yeye ni mwizi na munyanganyi.


Mimi ni mulango. Mutu akiingia kwa kupitia kwangu, ataokoka, ataingia na kutoka, naye atapata chakula.


Nanyi, ee kondoo wangu, ninyi ni watu wangu, nami ni Mungu wenu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Nasi watu wako, sisi kondoo wa kundi lako, tutakushukuru milele, na kukusifu nyakati zote.


Mujue kwamba Yawe ndiye Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, sisi ni mali yake; sisi ni watu wake na kondoo wake anaowachunga.


Maana yeye ni Mungu wetu. Sisi ni watu wake, kondoo wanaochungwa katika malisho yake. Heri leo mungesikiliza hivi anavyosema:


Sisi wote tumepotea kama kondoo, kila mumoja wetu ameelekea njia yake. Lakini Yawe alimubebesha azabu, ambayo sisi wenyewe tuliistahili.


Wataniomba wakuwe wengi kama kundi la kondoo wa kutolewa sadaka, kama kundi la kondoo katika Yerusalema wakati wa sikukuu zake. Hivi ndivyo miji yenu iliyokuwa ukiwa itakavyojaa makundi ya watu. Kwa hiyo watatambua kwamba mimi ni Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite