Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 10:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kondoo wale hawawezi kumufuata mugeni; lakini watamukimbia, kwa sababu hawajui sauti ya mugeni.”

Gade chapit la Kopi




Yoane 10:5
15 Referans Kwoze  

Ninajua matendo yako na taabu yako na uvumilivu wako. Ninajua kwamba hauwezi kuwakubali watu waovu. Umewapima wale wanaojiita mitume, kumbe si mitume, nawe ukatambua kwamba ni wasema uongo.


Yesu akawaambia tena: “Muangalie vizuri maneno munayosikia! Mungu atawapimia na kipimo kile munachowapimia wengine, na kuwaongezea hata zaidi.


Mwana wangu, ukiacha kusikiliza mafundisho, mara moja utapotea mbali na maneno ya maarifa.


Basi, sikuwaandikia kwa sababu hamujui ukweli, lakini kwa sababu munaujua na tena kwa sababu hakuna uongo wowote unaoweza kutokana na ukweli.


Lakini, Yosafati akasema: “Hapa hakuna nabii mwingine wa Yawe ambaye tunaweza kumwomba shauri?”


Watu hawa wametoka kati yetu, lakini hawakukuwa wa kundi letu, na kwa sababu hii wametuacha. Kama wangekuwa wa kundi letu, wangekaa pamoja nasi. Lakini wametuacha kusudi ionekane wazi ya kama hawakukuwa wa kundi letu.


Maana kutakuja wakati watu watakapokataa kusikiliza mafundisho ya kweli, lakini watafuata tamaa zao wenyewe wakijitafutia walimu wengi kwa kuwafundisha mambo yale wanayotamani kusikia.


“Basi mufanye angalisho na jinsi munavyosikia maneno. Kwa maana mutu anayekuwa na kitu, ataongezewa kingine, lakini mutu asiyekuwa na kitu, atanyanganywa kile anachozania kuwa nacho.”


Anapokwisha kuwatia hao kondoo wake inje, anawatangulia, nao wanamufuata kwa sababu wanajua sauti yake.


Niko na kondoo wengine wasiokuwa wa kundi hili. Ninapaswa vilevile kuwaleta, nao watasikia sauti yangu, na kutakuwa kundi moja na muchungaji mumoja.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite