Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 10:35 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

35 Maandiko Matakatifu hayawezi kuvunjwa. Mungu aliwaita ‘miungu’ wale walioambiwa neno lake.

Gade chapit la Kopi




Yoane 10:35
27 Referans Kwoze  

Mbingu na dunia vitatoweka, lakini maneno yangu hayatabadilika hata kidogo.


Kila mutu anapaswa kutii wakubwa wenye mamlaka. Maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; nao wakubwa wanaotawala wamesimikwa na Mungu.


Lakini ni vyepesi zaidi kwa mbingu na dunia kutoweka kuliko hata nukta moja ya Sheria kuondoshwa.


“Wandugu zangu, ilikuwa lazima yale Maandiko Matakatifu yatimie ambayo Roho Mutakatifu alitabiri kwa kinywa cha mufalme Daudi juu ya Yuda, yule aliyewaongoza wale waliomukamata Yesu.


Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Nao walipokwisha kumutundika juu ya musalaba, wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Kweli ninawaambia: kwa muda wote mbingu na dunia vitakapokuwa vingali, hakuna hata herufi moja wala nukta moja ya Sheria itakayoondoshwa mpaka yote yatimie.


Lakini neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: ‘Wewe umemwanga damu nyingi na kupigana vita kubwa. Kwa sababu ya damu nyingi ambayo umemwanga mbele yangu hapa katika dunia, hautanijengea nyumba.


“Kwenda umwambie mutumishi wangu Daudi: Yawe anasema hivi: Si wewe utakayenijengea nyumba ya kukaa.


Daudi akamwomba Yawe shauri: “Nikifuata kundi hili nitalikamata?” Yawe akamujibu: “Ulifuate maana utalipata na kuwaokoa hao waliotekwa.”


Hata alipomwomba Yawe shauri, Yawe hakumujibu kwa ndoto, kwa mawe ya kupiga kura, wala kwa njia ya manabii.


Samweli alimwambia Saulo: “Yawe alinituma kukupakaa mafuta kwa kukusimika kuwa mufalme wa watu wake Waisraeli. Sasa sikiliza maneno ya Yawe.


“Yawe, Mungu wenu atawachagulia nabii anayekuwa kama mimi kutoka kati yenu wenyewe, nanyi mutamutii huyo.


Kisha, Yesu akiwa anajua kwamba mambo yote yametimia, akasema hivi kusudi Maandiko Matakatifu yatimie: “Ninasikia kiu.”


Lakini nabii Yehu mwana wa Hanani, akakwenda kukutana na mufalme, akamwambia: “Unazani ni vema kuwasaidia waovu na kuwapenda wanaomuchukia Yawe? Mambo uliyofanya yamekuletea kasirani ya Yawe.


Yesu akawajibu: “Imeandikwa katika sheria yenu kwamba Mungu amesema: ‘Ninyi ni miungu.’


Kwa upande wangu, nilichaguliwa na Mungu na kutumwa naye katika dunia. Basi namna gani munasema kwamba ninamutukana Mungu kwa sababu nilisema kwamba mimi ni Mwana wa Mungu?


Basi tukio hilo lilitokana na ahadi ya Yawe kwa mufalme Yehu, kusema: “Wazao wako watatawala Israeli mpaka kizazi cha ine.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite