Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 10:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Baba yangu aliyenipa kondoo hawa ni mukubwa kuliko wote, na hakuna mutu anayeweza kuwanyanganya toka kwa Baba yangu.

Gade chapit la Kopi




Yoane 10:29
12 Referans Kwoze  

Wote Baba anaonipa wanakuja kwangu; nami sitamukataa hata kidogo yule anayekuja kwangu.


“Ninawaombea wao; siwaombei watu wa dunia, lakini hao ulionipa, kwa sababu wao ni wako.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Mumesikia jinsi nilivyowaambia kwamba ninajiendea, lakini nitawarudilia tena. Kama mungenipenda, mungefurahia kujua kwamba ninakwenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mukubwa kuliko mimi.


“Nimekujulisha kwa watu wale ulionipa, ukiwachagua katika dunia. Wao walikuwa watu wako, uliwatoa kwangu, nao walishika neno lako.


Mimi sitabaki tena katika dunia, lakini wao wangali katika dunia na mimi ninakuja kwako. Baba Mutakatifu, uwalinde kwa uwezo wa jina lako, lile jina ulilonipa, kusudi wakuwe mumoja kama vile sisi tunavyokuwa mumoja.


Alaaniwe mutu yeyote anayenidanganya, ambaye anaahidi kwa kiapo kunitolea sadaka ya nyama safi kutoka kundi lake, lakini ananitolea sadaka ya nyama mwenye kilema. Mimi ni mufalme mukubwa, na watu wa mataifa yote wananiogopa. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


Sasa ninajua kwamba Yawe ni mukubwa kuliko miungu yote, maana amewakomboa watu hawa toka katika mikono ya Wamisri ambao waliwatendea ubaya.”


Hivyo, nikaamuru wenye hekima wote wa Babeli waletwe mbele yangu kusudi wanielezee maana ya ndoto hiyo.


Yawe ni mukubwa, anastahili sifa nyingi; ukubwa wake hauwezi kuchunguzika.


Mimi ninawapa uzima wa milele, nao hawatapotea hata milele, wala hakuna mutu anayeweza kuwanyanganya toka katika mukono wangu.


Mimi na Baba yangu tuko mumoja.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite