Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 1:51 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

51 Yesu akaongeza kumwambia: “Kweli, kweli, ninawaambia: mutaona mbingu zimefunguka na wamalaika wa Mungu wakipanda na kushuka mpaka kwenye Mwana wa Mutu!”

Gade chapit la Kopi




Yoane 1:51
55 Referans Kwoze  

Akaota ndoto, na katika ndoto hiyo, aliona ngazi iliyosimamishwa juu ya dunia na incha yake inafika mbinguni. Wamalaika wa Mungu walikuwa wakipanda na kushuka katika ngazi hiyo.


Naye Stefano akasema: “Ninaona mbingu zimefunguliwa wazi, naye Mwana wa Mutu akisimama na mamlaka karibu na Mungu.”


Halafu malaika toka mbinguni alimutokea kwa kumutia moyo.


Mara moja kukaonekana kundi kubwa la wamalaika kutoka mbinguni wakiwa pamoja na yule malaika, wakimutukuza Mungu na kusema:


Yesu akajibu: “Mimi Ndiye! Nanyi mutamwona Mwana wa Mutu akiikaa na mamlaka kwa kuume kwa Mungu Mwenye Uwezo. Mutamwona vilevile akikuja katika mbingu katikati ya mawingu!”


Mara moja wakati Yesu alipotoka ndani ya maji, akaona mbingu zinafunguka na Roho Mutakatifu akishuka juu yake kwa mufano wa njiwa.


Yesu alipokwisha kubatizwa na kutoka ndani ya maji, mara moja mbingu zikafunguka, naye akamwona Roho wa Mungu akishuka kwa mufano wa njiwa na kukaa juu yake.


Kwa siku ya tano ya mwezi wa ine, mwaka wa makumi tatu, wakati nilipokuwa katikati ya wale watu waliopelekwa katika uhamisho, karibu na muto Kebari, mbingu zikafunguka, nikapata maono toka kwa Mungu.


Akaona katika maono mbingu imefunguliwa wazi, na kitu kimoja kinachokuwa kama nguo kubwa kikishuka, kikitelemushwa mpaka chini, kikishikwa kwenye pembe zake ine.


Watu wale wote walipobatizwa, Yesu akabatizwa vilevile. Alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka,


Basi Shetani akamwacha Yesu, nao wamalaika wakakuja kushugulika naye.


Kisha nikaona mbingu imefunguka na kukatokea farasi mweupe. Yule aliyepanda juu yake anaitwa Mwaminifu na Mwenye Ukweli, kwa maana anahukumu na kupigana vita kwa haki.


Nyuma ya mambo hayo nilipata maono mengine. Niliona mulango mumoja umefunguliwa wazi mbinguni. Halafu ile sauti niliyosikia mara ya kwanza, iliyolia kama baragumu, ikaniambia: “Panda huku, nami nitakuonyesha mambo yanayopaswa kutokea nyuma ya hayo ya mbele.”


na kuwapumzisha ninyi munaoteswa pamoja nasi. Jambo lile litatendeka wakati Bwana Yesu atakapoonekana tokea mbinguni pamoja na wamalaika wake wenye uwezo,


Na kwa rafla malaika wa Bwana akawatokea, na mwangaza wa utukufu wa Bwana ukawazunguka. Nao wakaogopa sana.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Yesu akasema: “Kweli, kweli ninawaambia: mutu asiyeingia kwa mulango wa upango wa kondoo, lakini anapandia na kuingilia nafasi ingine, yeye ni mwizi na munyanganyi.


Lakini zaidi ya hiyo Mwana wa Mutu ataikaa na mamlaka karibu na Mungu Mwenye Uwezo.”


“Wakati Mwana wa Mutu atakapokuja katika utukufu wake pamoja na wamalaika wote, ataikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu.


Ni Enoki, mutu wa kizazi cha saba tangu Adamu, ndiye aliyetabiri zamani juu yao, akisema: “Musikilize, Bwana atakuja pamoja na maelfu na maelfu ya wamalaika zake watakatifu.


Azabu yao itakuwa kuangamizwa kwa milele, na kutengwa mbali na uso wa Bwana na mbali na utukufu wa uwezo wake,


Kweli, kweli ninawaambia: yeye anayeniamini atafanya vilevile matendo ninayofanya. Na zaidi ya ile atafanya matendo makubwa kuliko haya, kwa sababu ninakwenda kwa Baba.


Kweli, kweli ninawaambia: anayeamini anapata uzima wa milele.


Walipokuwa wakifazaika kwa ajili ya jambo hili, mara moja watu wawili waliovaa nguo zenye kungaa wakawatokea.


Mwana wa Mutu atakufa sawa vile Maandiko Matakatifu yanavyosema juu yake, lakini ole kwa mutu yule atakayemutoa! Ingekuwa heri kwake kama asingezaliwa!”


Ninakuambia mambo ya kweli: wakati ulipokuwa kijana, ulijivalisha wewe mwenyewe na kwenda pahali ulipotaka. Lakini wakati utakapokuwa muzee, utanyoosha mikono yako na mutu mwingine atakuvalisha na kukupeleka pahali usipotaka.”


Kweli, kweli ninawaambia: kama mutu akishika maneno yangu, hatakufa hata milele.”


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: Musa hakuwapa ninyi mukate wa mbinguni, lakini ni Baba yangu anayewapa ninyi mukate wa kweli wa mbinguni.


Yesu akajibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu.


Kweli, kweli ninawaambia: mutalia na kusikitika, lakini watu wa dunia watafurahi. Mutahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.


Kweli, kweli ninawaambia: mutumishi si mukubwa kuliko bwana wake, wala mujumbe si mukubwa kuliko yule aliyemutuma.


Basi Yesu akaongeza kusema: “Kweli, kweli ninawaambia: mimi ni mulango wa upango wa kondoo.


Kwa hiyo Yesu akawaambia: “Kweli, kweli, ninawaambia: musipokula mwili wa Mwana wa Mutu na kunywa damu yake, hamutakuwa na uzima ndani yenu.


Vilevile amemupa Mwana mamlaka ya kuhukumu, kwa sababu yeye ni Mwana wa Mutu.


Basi Yesu akaongeza kuwaambia Wayuda: “Kweli, kweli, ninawaambia: Mwana hawezi kufanya kitu kwa mafikiri yake mwenyewe; anafanya tu kile ambacho anaona Baba akifanya. Na mambo yote Baba anayofanya, Mwana anayafanya vilevile.


Yesu akamujibu: “Kweli, kweli ninakuambia: mutu hawezi kuingia katika Ufalme wa Mungu asipozaliwa mara ya pili.”


Basi, ninataka mujue kwamba Mwana wa Mutu yuko na mamlaka ya kusamehe zambi hapa katika dunia.” Kwa hiyo akamwambia yule mutu mwenye kupooza: “Simama, utwae kipoyi chako na uende kwako.”


Yesu akamujibu: “Mbweha wako na makao yao ndani ya matundu, nao ndege wako na chicha, lakini Mwana wa Mutu hana nafasi ya kulala.”


Yawe wa majeshi anasema hivi: Amuka, ee upanga! Simama umushambulie muchungaji wangu, muchungaji anayenitumikia. Umuue muchungaji na kondoo watawanyike. Nitaunyoosha mukono wangu kwa kuwashambulia watu wazaifu.


“Siku ile itakapotimia, ninyi hamutaniuliza juu ya kitu fulani. Kweli, kweli ninawaambia: Baba atawapa chochote mutakachomwomba kwa jina langu.


Yesu akamujibu: “Hakika wewe ni tayari kutoa maisha yako kwa ajili yangu? Kweli, kweli ninakuambia: mbele jogoo hajawika, utakuwa umekwisha kunikana mara tatu.”


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: mbele Abrahamu hajazaliwa, mimi nilikuwa niko.”


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: kila mutu anayefanya zambi ni mutumwa wa zambi.


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: hamunitafuti kwa sababu muliona vitambulisho nilivyoonyesha, lakini kwa sababu mulikula mikate na kushiba.


Yesu akamujibu: “Unaamini kwa sababu nimekuambia kama nilikuona chini ya muti wa tini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite