Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 1:44 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

44 (Filipo alikuwa muzaliwa wa Betesaida, muji wa Andrea na Petro.)

Gade chapit la Kopi




Yoane 1:44
18 Referans Kwoze  

Basi wakamwendea Filipo wa kijiji cha Betesaida ya Galilaya na kumwambia: “Bwana, tunataka kuonana na Yesu.”


“Ole kwako, muji Korazini! Ole kwako, muji Betesaida! Kwa maana miujiza iliyofanyika ndani yenu ingalifanyika katika muji wa Tiro na muji wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuvaa magunia na kujipakaa majivu, kwa kuonyesha kwamba wamegeuka toka zambi zao.


Yesu akaendelea kusema: “Ole kwako muji Korazini! Ole kwako muji Betesaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika ndani yenu ingefanyika katika muji wa Tiro na wa Sidona, wakaaji wa kule wangekwisha zamani kuonyesha masikitiko yao kwa kuvaa magunia na kujipakaa majivu, na kugeuka toka zambi zao.


Mitume waliporudia toka kuhubiri wakamwelezea Yesu mambo yote waliyofanya. Kisha akaondoka pamoja nao na kwenda kwenye nafasi ya upekee karibu na muji Betesaida.


Yesu na wanafunzi wake wakafika Betesaida. Kule wakamuletea Yesu mutu mumoja kipofu na kumwomba amuguse kusudi apate kupona.


Pale pale Yesu akawalazimisha wanafunzi wake waingie ndani ya chombo na kumutangulia ngambo ingine ya ziwa la Galilaya kuelekea muji Betesaida. Kwa wakati ule alibaki akiaga lile kundi la watu.


Andrea na Filipo, Bartolomayo, Matayo, Toma, Yakobo mwana wa Alfayo, Tadeo, Simoni wa kundi la Wazeloti


kisha Filipo na Bartolomayo, Toma na Matayo aliyekuwa mulipishaji wa kodi; Yakobo mwana wa Alfayo, na Tadeo;


Walipofika katika muji wakapanda katika chumba cha gorofi walipokuwa wanazoea kukutanana. Na waliokuwa pale ni hawa: Petro, Yoane, Yakobo, Andrea, Filipo, Toma, Bartolomayo, Matayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni wa kikundi cha Wazeloti na Yuda mwana wa Yakobo.


Simoni (Yesu aliyemupa jina la Petro) na ndugu yake Andrea, Yakobo na Yoane, Filipo na Bartolomayo,


Siku iliyofuata Yesu alitaka kwenda Galilaya. Alipomukuta Filipo akamwambia: “Unifuate.”


Kisha Filipo akamukuta Natanaeli, akamwambia: “Tumemwona yule ambaye Musa aliandika habari zake katika kitabu cha Sheria na ambaye manabii walisema juu yake. Ni Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”


Natanaeli akamwuliza: “Kuna kitu kizuri kinachoweza kutoka Nazareti?” Filipo akamujibu: “Kuja uone.”


Natanaeli akamwuliza: “Unanijua namna gani?” Yesu akamujibu: “Filipo alipokuwa hajakuita, nilikuona wakati ulipokuwa chini ya muti wa matunda ya tini.”


Wakati Yesu alipoinua macho, akaona kundi kubwa la watu wakimufikia. Halafu akamwuliza Filipo: “Wapi tunaweza kununua vyakula kwa kulisha watu hawa?”


Filipo akamujibu: “Hata tukinunua mikate kwa bei ya vikoroti mia mbili vya feza, haitatosha kwa kumupa kila mutu hata kidogo tu.”


Filipo akaenda kumwambia Andrea, na kisha wote wawili wakaenda kumwelezea Yesu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite