Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, wala hakuna hata kitu kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.

Gade chapit la Kopi




Yoane 1:3
20 Referans Kwoze  

Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.


“Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili utukufu, heshima na uwezo, kwa maana wewe ndiwe uliyeumba vitu vyote; vile vimeumbwa na kupata kuwa kutokana na mapenzi yako.”


Mbingu ziliumbwa kwa neno la Yawe, na vyote vinavyokuwa ndani yake kwa pumzi ya kinywa chake.


Kisha Mungu akasema: “Tumufanye mutu kwa mufano wetu, anayefanana nasi, atawale samaki wa bahari, ndege wa anga, nyama wa kufugwa, dunia yote na viumbe vyote vinavyotambaa.”


Neno alikuwa yuko katika dunia, nayo dunia iliumbwa kwa njia yake, lakini ijapokuwa vile haikumutambua.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Ni mimi niliyeifanya dunia, na kuumba mwanadamu anayeishi humo. Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu, na kundi lote la nyota liko kwa amri yangu.


Ee Mungu wangu, usinihamishe sasa wakati ningali bado kijana. Ee Yawe, wewe unadumu milele.


Na hivi nipate kuwaelezea vema namna unavyotimia ule mupango uliokuwa umefichwa tangu zamani na Mungu, muumbaji wa vitu vyote.


Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia.


Nilikuwa pamoja naye kama fundi wa kazi, nilikuwa furaha yake kila siku, nikishangilia mbele yake siku zote,


Kwa mwanzo Neno alikuwa pamoja na Mungu.


Kwa njia ya imani tunafahamu kwamba ulimwengu uliumbwa kwa amri ya Mungu, hata vitu vinavyoonekana, viliumbwa kutoka vile visivyoonekana.


Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Laodikia hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeitwa ‘Amina’, mushuhuda mwaminifu, mwenye ukweli, na musingi wa viumbe vyote vya Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite