Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Yoane 1:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Hakuna mutu aliyemwona Mungu wakati wowote. Lakini Mwana wa pekee anayekuwa Mungu, anayeishi pamoja na Baba, huyu ndiye aliyemutambulisha kwetu.

Gade chapit la Kopi




Yoane 1:18
41 Referans Kwoze  

Kristo ni mufano kamili wa Mungu asiyeonekana. Yeye ni muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.


Si kusema kwamba kuna mutu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yule aliyetoka kwa Mungu; yeye ndiye aliyemwona Baba.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


“Baba yangu, umeweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana na yeyote ambaye Mwana anataka kumujulisha kwake.”


Hakuna hata mutu aliyekwisha kumwona Mungu wakati wowote. Tukipendana sisi kwa sisi, Mungu anaungana nasi na upendo wake unakamilika ndani yetu.


Ni yeye tu asiyeweza kufa na anayekaa katika mwangaza ambao mutu hawezi kukaribia. Hakuna mutu aliyemwona wala hakuna mutu anayeweza kumwona. Ndiye mwenye heshima na uwezo wa milele! Amina.


Hii ndiyo namna Mungu alivyoonyesha upendo wake kwetu: alimutuma Mwana wake wa pekee katika dunia kusudi kwa njia yake tupate uzima wa milele.


Tunajua vilevile kwamba Mwana wa Mungu amekwisha kuja, naye ametupatia ufahamu tupate kumujua Mungu anayekuwa wa kweli. Nasi tunaungana na yule Mungu anayekuwa wa kweli kwa njia ya Mwana wake Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli na uzima wa milele.


Kama mutu akisema “Ninamupenda Mungu,” naye anamuchukia ndugu yake, yeye ni mwongo. Kwa maana yule asiyemupenda ndugu yake anayemwona, hawezi kumupenda Mungu asiyemwona.


Nimekujulisha kwao, na nitaendelea kukujulisha kusudi upendo ule unaokuwa nao kwangu ukuwe ndani yao, nami mwenyewe nikuwe ndani yao.”


“Nimekujulisha kwa watu wale ulionipa, ukiwachagua katika dunia. Wao walikuwa watu wako, uliwatoa kwangu, nao walishika neno lako.


Yesu akajibu: “Filipo, nimekwisha kuwa nanyi siku nyingi sasa, nawe haujanijua bado? Aliyeniona mimi amemwona Baba. Basi sababu gani unasema: ‘Utuonyeshe Baba?’


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Kisha Yawe akasema nanyi kutoka katikati ya moto huo. Mukasikia maneno aliyosema lakini hamukumwona. Mulisikia tu sauti yake.


Mimi ninaongea naye kinywa kwa kinywa, waziwazi na si kwa kutumia mafumbo. Yeye ameliona umbo langu mimi Yawe. Kwa nini, basi, hamukuogopa kusema vibaya juu ya mutumishi wangu Musa?


Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliona kwa mbali utukufu wa Yesu, naye alisema habari zake.


Kwa Mufalme wa milele, asiyeweza kufa, asiyeonekana, Mungu peke yake, ikuwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.


Musikilize na kutii maneno atakayosema, wala musimwasi. Hatawasamehe uasi wenu maana nimemutuma kwa jina langu.


Basi, Hagari akamupa Yawe aliyezungumuza naye kule jina la “Wewe ni Mungu Anayeona,” kwa maana alifikiri: “Kweli hapa nimemwona yeye anayeniona?”


Siku moja Yoshua alipokuwa karibu na muji wa Yeriko, aliona kwa rafla mutu mumoja akisimama mbele yake na upanga uliochomolewa katika mukono wake. Yoshua akamwendea, akamwuliza: “Wewe ni wetu au ni wa waadui zetu?”


Wanawalilia wamama zao: Chakula kiko wapi, kinywaji kiko wapi? Wanazimia kama wale walioumizwa katika barabara za muji, na kukata roho katika mikono ya wamama zao.


Atachunga kundi lake kama muchungaji, atawakusanya wana-kondoo katika mikono yake, atawabeba kwa kifua chake, na atawaongoza polepole kondoo wanaonyonyesha.


Nilikuwa pamoja naye kama fundi wa kazi, nilikuwa furaha yake kila siku, nikishangilia mbele yake siku zote,


Yawe alipomaliza kuzungumuza na Abrahamu, akajiendea naye Abrahamu akarudi kwake.


Na kulikuwa mumoja wa wanafunzi ambaye Yesu alimupenda, na aliyekuwa akimwegamia Yesu pale kwenye chakula.


wakamwona Mungu wa Israeli. Chini ya miguu yake kulikuwa kitu kama sakafu ya mawe ya yakuti samawi, kikiwa safi kama mbingu inayoangaa.


Kweli, kweli ninakuambia: tunasema maneno tunayojua na kushuhudia maneno tuliyoona, lakini ninyi hamutaki kupokea ushuhuda wetu.


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite